BANDA MEDIA BLOG

MWILI WA MWENYEKITI WA UWT MKOA WA DODOMA SALOME KIWAYA WAAGWA NA KUSAFIRISHWA KWENDA NJOMBE KWA MAZISHI






Askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Dodoma Beatus Kinyaiya akiongoza ibada ya kuuaga mwili wa Marehemu Salome Kiwaya aliyepoteza maisha kwa ajali kabla ya kusafirishwa kwenda njombe kwa mazishi





Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda, Spika wa Bunge Job Ndugai, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Taifa [UWT] Sophia Simba na Waziri Wwa TAMISEMI George Simbachawene  wakiwa katika ibada hiyo IMETENGENEZWA NA BANDA BLOG
 

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Martha Mlata akizungumza jambo wakati alipokuwa akitoa salamu za Rambi rambi Kwenye Ibada hiyo ya Kumuaga Marehemu Salome Kiwaya

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma njini Christina Mndeme akitoa Pole

Mwenyekiti wa UWT Taifa Sophia Simba akishindwa kujizuia na kujikuta akiangua kilio  madhahuni wakati alipokuwa akimuelezea Mwenyekiti wa umoja huo mkoa wa Dodoma Salome Kiwaya aliopoteza uhai kwa ajili ya gari
Mwenyekiti wa UWT Taifa Sophia Simba akijiandaa kumhagi kwa ajili ya kumpa Pole Mzee Kiwaya Mara baada ya kutoa Salamu za Rambi rambi kutokana na kifo cha Mwenyekiti Umoja huo mkoa wa Dodoma Salome Kiwaya

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Adamu Kimbisa akimuelezea Marehemu Salome Kiwaya alivyokuwa ndani ya chama enzi za uhai wake

Mstahiki Meya wa manispaa ya Dodoma Jaffary Mwanyemba akizungumza kwenye ibada hiyo


Spika wa Bunge Job Ndugai akizungumza jambo wakati alipokuwa akitoa Pole kwa familia ya marehemu Salome kiwaya wakati wa ibada ya kuuga mwili wake iliyofanyika katika kanisa katoliki la Dodoma

Pinda akitoa Salamu za Rambi Rambi wakati waibada ya Kumuaga Mwenyekiti wa UWT Salome Kiwaya aliyefariki kwa ajali ya Gari  ijumaa iliyopita

Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda akimpa  mkoano wa pole Mzee Kiwaya kutokana na msiba wa mke wake salame Kiwaya wakati wa ibada ya kuuaga mwili wake iliyofanyika kanisa kuu katoliki la Dodoma ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho mjini Njombe
Familia ya Marehemu wakiwa kwenye Ibada hiyo






Mume wa Marehemu Salome Kiwaya, Mzee Kiwaya akitoa shukurani zake kwenye ibada hiyo

viongozi mbalimbali wakiwa katika ibada hiyo

Askofu Msaidizi wa kanisa hilo Chesco Msaga akitoa salamu za rambirambi wakati wa kuuaga mwili huo



Askofu wa kanisa hilo Mkoa huo Beatus Kinyaiya akitoa Baraka za mwisho mbele ya mwili wa marehemu Salome Kiwaya kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda njombe kwa ajili ya mazishi

Wakina mama wa chama cha Wanawake Wakataliki Tanzania Jimbo La Dodoma wakiusindikiza mwili wa Mwenyekiti wao ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa UWT mkoani humo Salome kiwaya mara baada ya ibada ya kuuaga Mwili kwa ajili ya Kuusafirisha kwenda mkoani njombe kwa ajili ya maziko
Maelfu ya wakazi wa Dodoma wakiwa nje ya kanisa kuu katoliki jimbo kuu la  mkoani humo wakiwa na huzuni wakati waliokuwa wakiusindikiza mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT uliyosafirishwa kwenda njombe kwa mazishi mara baada ya ibada ya kuuaga mwili wake

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG