| Pongezi ya kuhimu kidato cha sita huku wengine wakisheherekea na kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa
Na John Banda, Dodoma
MENEJA Biashara wa kampuni ya vinywaji ya SBC
Tanzania LTD [PEPS] tawi la Dodoma Abdala
Chuma amewaonya wanafunzi wa kidato cha sita kutotumia vibaya mitandao ya
kijamii katika kipindi hiki cha maandalizi ya mitihani ili kuepuka kufanya
vibaya wakati wa mitihani yao
Meneja huyo ameitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza kwenye mahafali ya wanafunzi wa
kidato cha sita wa shule ya Jamhuri sekondari ya mjini Dodoma ambapo amewata
kuitumia kwa kujiendeleza kitaaluma badala ya kujikita kwenye mambo yasiyo na
maadili
“Bado mwezi mmoja tu wa kujiandaa na mitihani hiyo
hivyo hakikisheni mnajiandaa kwa kusoma na wale mnaotumia mitandao ya kijamii
muitumie vizuri ili iwasaidie kufanya vizuri badala ya kubaki mkitumia
kuangalia picha za ngono, wasanii na mambo yasiyo na msingi”, alisema
Aidha Chuma amemshauri Mkuu wa shule hiyo kuziandika
changamoto zinaazowakabili kisha akabidhiwe mkuu wa kitengo cha uhusiano cha
SBC Tanzania makao makuu ili zifanyiwe kazi kwa kuwa kampuni hiyo kwa sasa
inarejesha faida wanazo pata kwa jamii kupitia miradi ya shule
Nae mkuu wa shule hiyo Mariam Hamis Lubuva amesema
changamoto walizo nazo ni pamoja na kukosekana kwa uzio, jengo la maktaba,
vitabu vya ziada na kiada, vifaa vya maabara kwa ajili ya mchepuo wa sayansi
ambapo kwa upande wa wanafunzi swala la utandawazi linasababisha wanafunzi kushuka
kitaaluma pamoja na kupolomoka kimaadili
|