Nairobi: Mwanafunzi wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka
16 kijiji cha Kwa-Kibathi Nchini Kenya amejiua baada ya Baba yake
kushindwa kumuhamisha Shule ya serikali aliyokuwa akisoma kumpeleka
shule binafsi. Kijana huyo alikuwa akisoma sekondari ya Maralal kwenye
County ya Samburu nchini Humo alikutwa amejinyonga kwa kamba pembeni mwa
nyumbani kwao.
Afisa wa polisi wa kaunti ya sambura OCPD Joseph Cheruiyot amesema
kuwa wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo licha ya baba yake
kueleza sababu za kujinyonga kwake kuwa ni kushindwa kuhamishwa shule