BANDA MEDIA BLOG

ACHENI MAJUNGU NA KIBURI KACHAPENI KAZI- DIWANI NITWA



NA JOHN BANDA, DODOMA

WANAWAKE kata ya Chamwino jijini Dodoma wametakiwa kuchapa Kazi zitakazowaletea maendeleo ya kiuchumi badala ya kukaa kwenye mikeka na kupiga soga za Umbea zisizo na faida

Pia wametakiwa kutokuwa na Kiburi kitakachowasababishia  Majivuno kiasi cha kuwavunjia Heshima Waume zao pindi mambo Yao la yatakapowanyookea.

Hayo Yamebainishwa na Diwani wa Viti Maalumu Jiji la Dodoma, Mary Nitwa wakati alipokuwa akiwaasa Wajasiriamali  zaidi ya 100, wa Kata ya Chamwino waliofudhu mafunzo ya kutengeneza bidhaa mbalimbali za Ujasiriamali yaliyofanyika katika  ukumbi wa Kanisa la Anglikana kwa kipindi cha wiki moja.

Diwani huyo Amewaambia Wajasiriamali hao ambao wengi wao ni wanawake, kwenda kuutumia vizuri Ujuzi walioupata kwenye mafunzo hayo  kwa kuanzisha Biashara zitakazowaongezea kipato, badara ya kupoteza Muda kwa kukaa kwenye vibaraza na mikeka huku wakipiga umbea na majungu yasiyo nafaida.

" Acheni mambo ya Umbea na kusemana hovyo, kaundeni vikundi fanyeni ubunifu wa biashara makachape Kazi Mpate baraka kwa Mungu, lakini angalizo langu mtakapofanikiwa nyie mlioopo kwenye Ndoa Msiwadharau waume zenu kutikana na kiburi cha mafanikio, Mungu hapendi ataondoa baraka zake bure", amesema na kuongeza.

Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Chamwino Jumanne Ngede,  ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi kwenye kufunga Mafunzo hayo amemuagiza Mtendaji wa kata na Afisa maendeleo ya jamii, kuhakikisha wajasiriamali hao Wanapata soko la kuuza Keki hasa kwenye sherehe zote zinazofanyika kwenye kata hiyo.

"Jiungeni vikundi watu wa Benki wapo hapa mkapewe mikopo yenye Riba ndogo, anzisheni biashara na wale wanaotengeneza Keki hata Kama wote hapa, nawaagiza kata muwatengenezee mazingira hawa kwenye sherehe zote zikiwemo harusi hawa ndiyo watengeneze na kuuza keki", amesema

Ameongeza kuwa kufanikiwa siyo kigezo cha kiburi na dharau kwawenzi katika ndoa “mimi hapa nilipo nina mashine a kusaga katika meneo mbalimbali, nina magari ya kutembelea na kufanyia kazi, hata fedha si haba ninazo lakini mbana sigombani na mama yenu pale nyumbani, na nyie mkizipata msije makaota mapembe kwa wenzi wenu zitakuja kukimbia bure ninawaonya”, amesema




Sehemu ya Wahitimu wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini



Sehemu ya Wahitimu wa mafunzo hayo wakakabidhiwavyeti vya ushiriki na Diwani wa Kata ya Chamwino Jumanne Ngede
 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG