BANDA MEDIA BLOG

WANANCHI WAACHE KUOGOPA WANAPOTENDEWA NDIVYO SIVYO MAHAKAMANI- BI. ALISIA

NA JOHN BANDA, DODOMA

TUME ya Utumishi wa Mahakama imewaelekeza Wananchi wenye malalamiko ya Ukiukwaji wa maadili yaliyosababisha kutotendewa haki katika Maamuzi ya Kimahakama na baadhi ya Maafisa Mahakama (MAHAKIMU) kuandika Barua na kuiwasilisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa..

 Akiongea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma ambako Maadhamisho ya wiki ya Sheria yanafanyika, Naibu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama (Nidhamu na Maadili) Bi. Alesia Mbuya amewataka wananchi kutokuwa na wasiwasi wanapoona hawakutendewa haki na Mahakimu kutokana na ukiukwaji huo.

Bi. Lesia amesema Wanachi wanapaswa Kuandika Barua za Malalamiko hayo na kuziwasilisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa au Wakili anayetoka  ofisi ya Mwanasheria Mkuu Serikali.

Amesema barua hiyo ikishapokelewa na katibu wa kamati ya Maadili ikawa imekithi vigezo vikiwemo kusainiwa na Mlalamikaji   na kisha hufanyiwa uchunguzi dhidi ya Hakimu mlalamikiwa, baada ya hapo Jarada hufikishwa mbele ya Wajumbe wa Tume wa maadili kwa ajili ya Kufanyiwa maamuzi 

" Mwananchi asiwe na woga, kama anaona hakutendewa haki mahakamani na Hakimu kutokana na ukiukwaji wa maadili, aandike barua ya malalamiko kisha aifikishe Ofisi ya Mkuu wa mkoa kwa Katibu  Tawala itafanyiwa kazi na kamati kisha italetwa tume na kufanyiwa maamuzi", amesema

Aidha amesema inapobainika Hakimu amekiuka Maadili ya Utumisha wa mahakama kuna hatua anachukiwa ikiwemo, kufukuzwa Kazi, kusimamishwa au kuonywa hivyo wananchi wasisite.

Naibu katibu Huyo amesema Tume hiyo Imeundwa kwa ajili ya kuimarisha maadili ya Maafisa mahakama (Mahakimu), ambapo tume hiyo ina wajibu wa kuziimalisha kamati za maadili kwa kuzijengea uwezo ili ziweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria.

 Aidha amesema Changamoto ambayo Tume inakumbana nayo  katika utekelezaji wa majukumu Yake, ni pamoja na Wananchi kutofahamu vema majukumu ya  Tume hiyo, pamoja na kamati zake, hali inayosababisha  wananchi wenye malalamiko dhidi ya ukiukwaji wa Maadili kwa Mahakimu, kutojua Utaratibu na Sehemu Sahihi za kuwasilisha malalamiko Yao dhidi ya ukiukwaji huo.






 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG