AFGHANSTAN: Maofisa wa serikali nchini
Afghanstan
wamearifu kuwa watu hamsini, wakiwemo wanawake na watoto wameuawa na
askari upande wa Jimbo la kaskazini mwa mji wa Sar-e-Pul. Naye msemaji
wa gavana wa jimbo hilo ameiambia BCC kwamba Wapiganaji walikishambulia
kituo cha ukaguzi wa usalama katika eneo la Mirzawalang na kuingia
kijijini, kisha kushambulia kituo cha polisi cha eneo hilo ambapo
wanawake na watoto ni miongoni mwa waathirika.

Msemaji
huyo aliendelea kueleza kuwa anaamini kuwa washambuliaji hao wahusika
wakuu ni muungano wa makundi ya wapiganaji wa Taliban na wanamgambo wa
kunid la Islamic State ingawa wapiganaji wa kundi la Taliban wamekana
madai hayo ikiwemo mauaji ya raia.

Taarifa zaidi zinadai kuwa wajumbe ishirini na nane wa wanamgambo wanaoiunga mkono serikali waliuawa.
#BBCswahili