Wanawake
wakiwa wamevalia khanga ambayo ndio ilikuwa dress code ya tamasha
walikusanyika kwa wingi kwa ajili ya kupata mafunzo na ushauri bila
kusahau burudani.
Jumapili
iliyoisha ya tarehe 08.11. 2015, wanawake mbali mbali jijini Dar es
salaam walikutana katika tamasha la kitchen party gala likiwa limebeba
ujumbe wa mwanamke simama na timiza ndoto zako.
Ilichezeshwa
droo ya kushinda safari ya Afrika Kusini kwa siku mbili alishinda,
iliyodhaminiwa na kinyago tours. Pamoja na droo ya kumtafuta Mshindi wa
safari ya Mikumi national park nae alipatikana akapokea certificate toka
kwa mkurugenzi wakinyago tours bi Diana
Pichani juu ni washiriki wa kitchen party gala wakifuatilia mafunzo kwa umakini.
 |
|
Mkurugenzi
wa kinyago tours bi Diana nae alitoa funzo la kufanya kazi kwa malengo
hata kama umeajiriwa malengo yako ni yapi?leo ukiachishwa kazi ghafla
umejipangaje? ana miaka 27 tu lakini anamiliki kampuni yake ya Tours and
safars. |
 |
|
Msemaji
Bi Maida Waziri mkurugenzi wa Ibra Contractors nae alishirikisha
wanawake safari yake ya mafanikio toka akiwa fundi cherehani mpaka sasa
anamiliki kampuni kubwa ya ujenzi wa majengo na bara bara.Aliwasisitiza
wanawake kujiamini na kutokuogopa kuthubutu ukijiamini popote unapenya
lakini lazima uwe na malengo na mikakati. |