BANDA MEDIA BLOG

ROSE MUHANDO KUOLEWA NA ASKOFU MKENYA

 

MALIKIA wa nyimbo za injili Nchini Tanzania Rose Muhando anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni huko nchini Kenya na  mwimbaji mwenzake wa nyimbo za injili.

kwa mujibu wa mitandao ya kijamii nchini humo Malikia huyo anatarajia kuolewa na Bishop, Robert Bob Lumbasi ambapo Bishop huyo ametoa tangazo rasmi kuwa, Rose Mhando hayuko sokoni tena bali kwa sasa anasubiri kuolewa kwani kila kitu kipo tayari, na kwamba hata mahali tayari zilishatolewa zote

Imebainishwa katika vyanzo hivyo kuwa Wapenzi wa Muziki wa Injili wa wawili hao, wanasubiri kwa hamu  Tarehe ya harusi hiyo, ambayo inatajwa kuwa itakuwa ya kukata na shoka kwani watarajiwa hao ni watu maarufu huku Bob akitajwa kuwa ni Afisa wa Polisi, Bishop na mwimbaji nguli wa nyimbo za injili nchini humo.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG