BANDA MEDIA BLOG

HII NI VITA YA AMISSI NA HAMISI, SASA KILA MMOJA ANA MABAO 14 KIBINDONI


Mechi mbili za Ligi Kuu Bara za watani, Yanga na Simba zimeisha na kila upande unasherekea kivyake.

Simba imeshinda kwa mabao 5-1 dhidi ya Mgambo Shooting, lakini Yanga wamekwama kwa Prisons baada ya kulazimisha sare ya mabao 2-2 wakiwa ugenini mjini Mbeya.

Lakini kikubwa hapa ni mshambuliaji Hamisi Kiiza kufikisha mabao 14 sawa na Amissi Tambwe wa Yanga ambaye pia ana idadi hiyo.

Pamoja na kukosa penalti leo, lakini Kiiza amefunga mabao mawili katika ushindi huo wa Simba wa mabao 5-1.


Kiiza amefunga moja katika sare ya 2-2, lakini anaonekana hakutaka kupiga mkwaju wa penalti ambayo ilipigwa na Msuva.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG