BANDA MEDIA BLOG

WANANCHI WAASWA KUTOKUVAMIA MAENEO YA VIWANJA KIHOLELA KWANI WANACHANGIA MIGOGORO YA ARDHI

images modified
NA VICTOR MASANGU, KISARAWE
…………………………………………………
JAMII hapa nchini imetakiwa kuachana na vitendo vya kuvamia  mashamba na viwanja vya waatu kiholela  bila ya kuzingatia na taratibu na  zilizizowekwa  kwani kufanya hivyo kunachangia kwa kiasi kikubwa  kuchochea vurugu na na uvunjifu wa amani kutokana na kuwepo kwa migogoro ya ardhi.
Hayo yamesemwa na  Afisa mtendaji wa Tarafa ya Sungwi iliyopo Wilayani Kisarawe, Mkoa wa Pwani  Thomas Mollel wakati alipokuwa akijibu malalamiko kwa waandishi wa habari yaliyoyotolewa na  baadhi ya wananchi wa kiluvya ‘B’ kuhusina na suala la uvamizi wa maeneo yao ya viwanja  kinyume na taratibu.
Mollel alisema kwamba anashangazwa kuona baadhi ya wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria wenyewe kwa kuvamia maeneo ya watu na kuanza kufanya ujenzi kitu ambacho kimesababisha kuwepo kwa hali ya uvunjifu wa amani, ambapo ameongeza hawezi kuifumbia macho na atalivaia njuga suala hio hili haki iweze kutendeka kwa kila mtu  mwenye eneo lake kihalali.
“Kwa kweli mimi sipendi kuoana  wanannchi wanavunja sheria ambazo zimewekwa kwa kuamua kuvamia maeneo ya watu na kuanz akufanya ujenzi hii sio sahihi kwani kufanya hivyo mwisho wa siku kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani kutokaja na kuibuka kwa migogoro hiyo ya ardhi kwa ahiyo naomba waachane na tabia hiyo,” aisema Mollel.
Aidha Afisa Mtendaji huyo alibainisha kwamba wananchi wanapswa kubadiika na kuzingatia sheria za nchi ziizowewekwa ii kuepekuna na hali ya kugombania maeneo ya viwanja na mashamba  kitu amabcho amedai ni kitendo cha kujichukulia sheria mikononi.
Kwa upande wake mmoja wa wananchi ambao wameingia katika mgogoro mkubwa kutokana na eneo lake kuvamia anayejulikana kwa jina la Januaris Maganga alimwomba Waziri mwenye dhamana kuliingilia kati sakata hilo kwani kwa sasa limedumu kwa muda mrefu bila ya kutafutia ufumbuzi jambo ambalo linamweka katika hali ya kuishi kwa mashaka kutokana na vitisho anavyovipata kwa sasa.
“Mimi nina eneo langu kama hekai mbili na nusu lakini nashangaa kuna mzee mmoja ameamua  kulivamia kinyume cha sheria kabisa wakati mimi eneo hii ni langu kihaai na nina hati ambayo ninayo lakini bado analeta ukorofi kwa hiyo mimi hai kama hii inabadi waziri mwenye dhamana atusaidie ili tuweze kutatua mgogoro huu na mimi niweze kupata haki yangu,”alisema Maganga.
Naye mmoja wa wazee wa siku nyingi katika kijiji hicho cha kiluvya ‘B; Rashid Kilusungu akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake kuhusina na tabia ya wananchi kuvamia maeneo kiholela alisema sio jambo zuri kwani linaweza kuchochea kutokea kwa vurugu hivyo ni vema busara zikatumika ili hali ya amani na upendo iwepo.
MIGOGORO ya viwanja na mashamba katika maeneo ya Wilaya ya Kisarawe bado inaonekana kuwa ni sugu kutokana na mamlaka ambazo zinahusika zinachangia kwa kiasi kikubwa kutokana na kuchelewesha kutoa hati za wamiliki halali wa maeneo hayo, hali ambayo inasababisha wananchi kuamua kuvamia na kujenga bila ya kuwa na kibali halali.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG