Tumefarijika kuona takwimu za
wiki iliyopita kuanzia tarehe 16 hadi 22 Mei 2016 zinazoonyesha kuwa,
kasi ya ugonjwa wa kipindupindu imepungua kwa asilimia 49 (karibu nusu
ya wagonjwa), ambapo idadi ya wagonjwa wapya walioripotiwa ni 108, na
hakuna aliyepoteza maisha, ikilinganishwa na wagonjwa wapya 212
walioripotiwa wiki iliyotangulia ya Mei 9 hadi 15.
Mikoa ambayo imeripoti wagonjwa
wiki hii ni Morogoro (47), Manyara(16), Lindi (14), Mara (11) Dar es
Salaam (9), Pwani (6), Kagera (2), Kilimanjaro (2) na Iringa (1).
Halmashauri zilizoongoza kutoa
wagonjwa wengi ni Kilosa (27), Mvomero (15), Kilwa (14), Tarime Mjini
(11), Babati Vijijini (10), Kinondoni (9), Babati Mjini (5), Morogoro
Mjini (5), Kibaha Mjini (4), Bukoba Mjini (2), Chalinze (2), Same (2),
Iringa Mjini (1) na Mbulu (1).
Katika wiki iliyopita, mikoa
ambayo haikuwa na wagonjwa wa kipindupindu ni Kigoma, Dodoma, Mwanza,
Geita, Singida, Shinyanga, Arusha, Tanga, Tabora, Rukwa, Katavi, Mbeya,
Simiyu na Mtwara. Na mikoa ambayo haijawahi kuripoti mgonjwa wa
kipindupindu tangu mlipuko uanze ni Ruvuma na Njombe
Kupungua kwa idadi ya wagonjwa
kusirudishe nyuma juhudi za kuuzuia ugonjwa huu, bali tunatakiwa
kuzidisha jitihada ili tuweze kuuondoa, tusiwe na wagonjwa kabisa. Ni
vema kuchukua tahadhari zaidi, hasa katika msimu wa masika, ambapo kuna
uwezekano mkubwa wa maji ya mvua kusambaza vimelea vya ugonjwa huu.
Tuendelee kuzuia maambukizi, na pia kuendelea kutoa taarifa za ugonjwa
kila siku, hata kama hakuna wagonjwa, na kusimamia kikamilifu hatua
mbalimbali za udhibiti wa mlipuko huo
Tags
AFYA