MOSHI SHABANI MALLEMA
Tanzania ni moja ya nchi
pekee Duniani iliyofanikiwa kuilinda na kuitunza Amani yake iliyoasisiwa
na viongozi wake wakuu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Amani Abeid
Karume, hivyo kwa kwakuzingatia hayo Mkuu wa Wilaya mpya ya Kigamboni
Hashimu Shaibu Mgandilwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na
Usalama, amezungumza na wanakigamboni kuhusu Amani hiyo na kutoa
tahadhari.
Ambapo ameeleza kuwa hivi
karibuni wamejitokeza watu wachache wasio litakia mema taifa la Tanzania
kwa maslahi yao binafsi na kuona amani iliyopo haina thamani
wakiwashawishi watu kuandamana wakati familia zao wame zisafirisha
kwenda nje ya nchi.
Hivyo Mkuu wa Wilaya ya
Kigamboni na akiwa kama Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama katika Wilaya
yake amewaomba wananchi wa Kigamboni vijana kwa wazee, wanawake kwa
wanaume na makundi yote ya kijamii katika wilaya yake kuendelea kuilinda
na kuitunza Amani ya nchi, kama ilivyo asisiwa na viongozi waanzilishi
wa Taifa hili mpaka hii leo wanafurahia maisha yao yenye utulivu.
Huku akiwaasa Wanakigamboni wote kwa kuwataka kutokushiriki katika vitendo vya aina yeyote vyenye mlengo wa kuvuruga Amani, ikiwemo maandamano yasiyo na tija kwa taifa na maisha ya watanzania.
Tags
HABARI KITAIFA