BANDA MEDIA BLOG

UFUNGUZI WA MICHEZO YA OLIMPIKI YA RIO2016 WAFANA BRAZIL

Fataki za aina mbali mabli zilirushwa katika ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki nchini Brazil usiku wa kuamkia leo ambapo fainali hizo za michezo ya Olimpika imeanza (CHANZO BBC)
bra
5.55am:Fataki zinawashwa katika uwanja huo
fataki Rio
5.50am:Na mwenge wa Olympic uliowasili katika uwanja wa Mariccana unapokezwa aliyekuwa mwanariadha wa mbio za Marathon nchini Brazil Vanderlei Cordeiro de Lima – Ambaye anauwasha mwanga katika uwanja huo ishara ya ufunguzi rasmi ya michezo hiyo.
Mwanga wa michezo ya Olimpiki wawashwa
Mwanga wa michezo ya Olimpiki wawashwa
5.32am:Wimbo wa taifa la Brazil unaimbwa kwa sasa katika ukumbi wa ufunguzi wa michezo hiyo5.20am:Uwanja wa Mariccana ulivyofurika maelefu ya mashabiki
Uwanja wa Mariccana
Uwanja wa Mariccana
5.15am:Bendera zote zimewekwa pamoja kuonyesha ishara ya umoja uliopita baina ya mataifa mbali mbali duniani yanayoshiriki michezo hiyo
Bendera zote zawekwa pamoja
Bendera zote zawekwa pamoja
5.05am: Na sasa kikosi cha wanariadha wakimbizi pia kinaingia hapa.Baadhi ya wanariadha hawa walikuwa kule nchini Kenya wakifanya mazoezi tayari kwa maandalizi ya michezo hii.
5.00am:Kikosi cha wanariadha kinaingia kikiongozwa na bingwa katika mchezo wa tenisi Andy Murray
Wanariadha wa Uingereza waingia katika uwanja wa Mariccana wakiongozwa na bingwa wa mchezo wa tenisi Andy Murray
Wanariadha wa Uingereza waingia katika uwanja wa Mariccana wakiongozwa na bingwa wa mchezo wa tenisi Andy Murray
4.55am:Vilevile kuna raia wa Brazil ambao licha ya kushimndwa kuhudushuria ufunguzi wa michezo hiyo waliamua kutafuta eneo la juu kama vile milima ili kushuhudia yanayoendelea.
Raia wa Brazil wakiangalia yanyoendelea kwa mbali
Raia wa Brazil wakiangalia yanyoendelea kwa mbali
4.45am: Na sasa ni wanariadha wa Afrika Kusini wanaoingia katika uwanja wa Mariccana
Wanariadha wa Afrika Kusini wakiimbia na mbwembwe
Wanariadha wa Afrika Kusini wakiimbia na mbwembwe
4.35am:Wanariadha wa Jamaica wakipita mbele ya mashabiki.Kumbuka ni taifa hili ambalo lina mwanariadha aliye bingwa wa mbio za mita 100 duniani Usain Bolt.
Wanamichezo wa Jamaica
Wanamichezo wa Jamaica
4.30am:Hao wanaoonekana mbele ya mashabiki sasa ni wanamichezo wa taifa dogo la Lesotho lililopo kule Afrika ya Kusini
Wanariadha wa taifa la Lesotho nao pia hawakuwachwa nyuma
Wanariadha wa taifa la Lesotho nao pia hawakuwachwa nyuma
4.15am:Wachezaji wa Marekani ndio hao wanaingia uwanjani
Wanariadha wa Marekani wakiingia uwanjani.Muogeleaji Michael Phelps ndio mbeba bendera wao
Wanariadha wa Marekani wakiingia uwanjani.Muogeleaji Michael Phelps ndio mbeba bendera wao
4.10am:Aliyekuwa mchezaji nambari wa mchezo wa tenisi kwa upande wa akina dada Caroline Wozniacki ndiye anayebeba bendera ya taifa la Denmark.
kikosi cha wachezaji wa Denmark chaingia uwanjani Mariccana
kikosi cha wachezaji wa Denmark chaingia uwanjani Mariccana
4.00am: Eneo la katikati la uwanja wa Mariccana limeanza kujaa wachezaji kutoka mataifa mbali mbali.
3.45am:Mwandishi wa BBC Peter Okwoche amekuwa akizungumza na wakaazi wa Rio ambao wamekuwa wakikongamana katika ukumbi wa Fonzona ili kuangalia sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo .
Marina anasema kuwa kile anachokiona ni kitu ambacho hajawahi kushuhudia maishani mwake.”Sijui iwapo wakati huu ni mzuri wa sisi kuwa na michezo hii ,kwa sababu tuna matatizo mengi.Lakini nahisi nafurahi kuwa hapa ili kushuhudia ikifanyika katika taifa langu.
Sijui iwapo raia wa Brazil wataiunga mkono lakini najua watafurahia,na pengine baadaye tutakuwa na matumaini na taifa letu”.
Bendera ya Brazil ikipepea nje ya ukumbi wa sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo
Bendera ya Brazil ikipepea nje ya ukumbi wa sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo
3.15am:Wanamichezo wa taifa la Australia wakipita mbele ya mashabiki
Wanariadha wa Australia wakiingia katika uwanja wa Mariccana
Wanariadha wa Australia wakiingia katika uwanja wa Mariccana
3.10am:Baadhi ya Mashabikio waliotumia usafiri wa aiana mbali mbali ili kuhakikisha kuwa wanahudhuria sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo.
baadhi ya mashabiki waliohudhuria sherehe hizo
baadhi ya mashabiki waliohudhuria sherehe hizo
2.50am:Kikosi cha wanariadha wa Olimpiki kutoka Ugiriki ndio hao wanapita mbele ya mashabiki wanaowapongeza
Wanariadha wa Ugiriki
Image captionWanariadha wa Ugiriki
2.45am:Tayari mataifa yanayoshiriki yameanza kuingia katika uwanja wa Mariccana huku shangwe na nderemo zikipamba hewani.
20.30am:Fataki zilizorushwa katika ufunguzi wa michezo ya Rio2016
Fataki za aina mbali mabli zilirushwa katika ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki nchini Brazil
2.15am: Usalama uliimarishwa nje ya ukumbi wa ufunguzi wa michezo hiyo katika eneo la Barra huku vikosi vya kijeshi vikisambazwa katika kila eneo la mita 25.msongamno wa magari sio mkubwa usiku huu.Inaonekana kwamba wakaazi wa Rio wanafuatilia ufunguzi katika runinga zao majumbani mwao!
Usalama umeimarishwa katika ukumbi wa ufunbguzi wa michezo hiyo
Image captionUsalama umeimarishwa katika ukumbi wa ufunguzi wa michezo hiyo

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG