Fataki
za aina mbali mabli zilirushwa katika ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki
nchini Brazil usiku wa kuamkia leo ambapo fainali hizo za michezo ya
Olimpika imeanza (CHANZO BBC)
5.32am:Wimbo wa taifa la Brazil
unaimbwa kwa sasa katika ukumbi wa ufunguzi wa michezo hiyo5.20am:Uwanja
wa Mariccana ulivyofurika maelefu ya mashabiki
5.15am:Bendera zote zimewekwa
pamoja kuonyesha ishara ya umoja uliopita baina ya mataifa mbali mbali
duniani yanayoshiriki michezo hiyo
5.05am: Na sasa kikosi cha
wanariadha wakimbizi pia kinaingia hapa.Baadhi ya wanariadha hawa
walikuwa kule nchini Kenya wakifanya mazoezi tayari kwa maandalizi ya
michezo hii.
5.00am:Kikosi cha wanariadha kinaingia kikiongozwa na bingwa katika mchezo wa tenisi Andy Murray
4.55am:Vilevile kuna raia wa
Brazil ambao licha ya kushimndwa kuhudushuria ufunguzi wa michezo hiyo
waliamua kutafuta eneo la juu kama vile milima ili kushuhudia
yanayoendelea.
4.45am: Na sasa ni wanariadha wa Afrika Kusini wanaoingia katika uwanja wa Mariccana
4.35am:Wanariadha wa Jamaica
wakipita mbele ya mashabiki.Kumbuka ni taifa hili ambalo lina
mwanariadha aliye bingwa wa mbio za mita 100 duniani Usain Bolt.
4.30am:Hao wanaoonekana mbele ya mashabiki sasa ni wanamichezo wa taifa dogo la Lesotho lililopo kule Afrika ya Kusini
4.15am:Wachezaji wa Marekani ndio hao wanaingia uwanjani
4.10am:Aliyekuwa mchezaji
nambari wa mchezo wa tenisi kwa upande wa akina dada Caroline Wozniacki
ndiye anayebeba bendera ya taifa la Denmark.
4.00am: Eneo la katikati la uwanja wa Mariccana limeanza kujaa wachezaji kutoka mataifa mbali mbali.
3.45am:Mwandishi wa BBC Peter
Okwoche amekuwa akizungumza na wakaazi wa Rio ambao wamekuwa
wakikongamana katika ukumbi wa Fonzona ili kuangalia sherehe za ufunguzi
wa michezo hiyo .
Marina anasema kuwa kile
anachokiona ni kitu ambacho hajawahi kushuhudia maishani mwake.”Sijui
iwapo wakati huu ni mzuri wa sisi kuwa na michezo hii ,kwa sababu tuna
matatizo mengi.Lakini nahisi nafurahi kuwa hapa ili kushuhudia
ikifanyika katika taifa langu.
Sijui iwapo raia wa Brazil wataiunga mkono lakini najua watafurahia,na pengine baadaye tutakuwa na matumaini na taifa letu”.
3.15am:Wanamichezo wa taifa la Australia wakipita mbele ya mashabiki
3.10am:Baadhi ya Mashabikio
waliotumia usafiri wa aiana mbali mbali ili kuhakikisha kuwa
wanahudhuria sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo.
2.50am:Kikosi cha wanariadha wa Olimpiki kutoka Ugiriki ndio hao wanapita mbele ya mashabiki wanaowapongeza
2.45am:Tayari mataifa yanayoshiriki yameanza kuingia katika uwanja wa Mariccana huku shangwe na nderemo zikipamba hewani.
20.30am:Fataki zilizorushwa katika ufunguzi wa michezo ya Rio2016
2.15am: Usalama uliimarishwa nje
ya ukumbi wa ufunguzi wa michezo hiyo katika eneo la Barra huku vikosi
vya kijeshi vikisambazwa katika kila eneo la mita 25.msongamno wa magari
sio mkubwa usiku huu.Inaonekana kwamba wakaazi wa Rio wanafuatilia
ufunguzi katika runinga zao majumbani mwao!
Tags
MICHEZO KIMATAIFA
