BANDA MEDIA BLOG

MECHI 7 KALI ZA KIHISTORIA KATI YA STARS VS NIGERIA


DSC_0050
Na Athumani Adam
Stars na Nigeria zinakutana kwa mara ya nane kwenye mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu Afcon 2017. Japokuwa ni mchezo wa kukamilisha ratiba baada ya timu ya Misri kuwa tayari imefuzu kutoka kwenye Kundi G, lakini Stars  inatafuta rekodi kwa kuifunga Nigeria kwa mara ya kwanza katika ngazi ya timu za wakubwa.
Kabla ya mechi ya leo Stars na Nigeria zimekutana mara saba (7), Nigeria imeshinda mara nne (4) na kutoka sare mechi tatu (3).  Makala hii inakupa kumbukumbu ya mechi zote saba baina ya mataifa haya

  1. Nigeria 1 – 1 Tanzania, FIFA World Cup Qualifier (6 December 1980)
Ilikuwa ni kampeni ya kutafuta timu ambazo zitawakilisha bara la Afrika kwenye kombe la dunia 1982 kule nchini Spain. Hii ilikuwa mechi ya kwanza hatua ya raundi ya pili. Mudashiru Lawal aliifungia Nigeria Dakika 29, Mohamed Salim akasawazisha dakika ya 85.
Kikosi cha stars kilikuwa: Juma Pondamali, Thuwein Ally (sub Kajole), Ahmedi Amasha, Yusufu Bana, Charles Boniface, Omar Hussein(sub Peter Tino) , Juma Mkambi, Jella Mtagwa, Mohammed Rishard, Mohammed Salim, Leodger Tenga
  1. Tanzania 0 – 2 Nigeria, World Cup Qualifier (20 December 1980)
Kila Mtanzania kipinde kile aliamini Stars itaiondoa Nigeria kwenye mashindano. Ari ilikuwa kubwa sababu ya sare kwenye mchezo wa kwanza kule jijini Lagos. Lakini Tanzania ilijikuta ikipoteza mchezo nyumbani kwenye uwanja wa taifa (Uhuru stadium)
Kikosi cha stars  kilikuwa: Juma Pondamali, Thuwein Ally, Yusufu Bana ( sub Mohamed Rishrad), Isihaka Hassan, Omar Hussein, Mohamed Kajole, Juma Mkambi, Jela Mtagwa, Hussein Ngulungu (sub Charles Boniface), Mohammed Salim, Peter Tino
  1. Nigeria 3 – 1 Tanzania, Africa Cup of Nation (8/3/1980)
Tanzania ilikuwa na miongoni mwa timu nane zilizofuzu kwenye fainali za mataifa Afrika ambazo zilifanyika nchini Nigeria. Tanzania ilipangwa kundi A pamoja na timu za Misri, Ivory Coast na mwenyeji Nigeria.
Kwenye mashindano hayo Tanzania ilipoteza mchezo dhidi ya Nigeria ambayo ilikuwa ni mechi ya ufunguzi. Pia Tanzania ilipoteza tena  dhidi ya Misri 2-1 na kutoka sare dhidi ya Ivory Coast kwenye mechi ya mwisho.
Kwenye mechi dhidi ya Nigeria kikosi cha Tanzania kilikuwa: Othumani Mambosasa, Mohamedi Kajole, Jela Mtagwa, Ledger Tenga, Tasso Mukebezi, Omar Hussein, Juma Mkambi(mfungaji wa bao), Ngulungu, Massewa, Ramadhani, Waziri (sub Peter Tino)
  1. Nigeria 2 – 1 Tanzania, All Africa game (12 January 1973)
Mwaka huu Nigeria walipata fusra ya kuandaa mashindano ya all African game. waliibuka mabingwa kwa upande wa soka na kupata medali ya dhahabu. Tanzania ilipoteza kwa Nigeria  kwenye mechi ya Kundi A ambalo lilikuwa na timu za Ghana, Nigeria, Tanzania na Algeria.
Kwenye mashindano haya Tanzania ilifanikiwa kupata medali moja ya dhahabu baada ya mwanariadha Filbert Bayi kushinda mbio za mita 1500.
  1. Tanzania 0 – 0 Nigeria, Afcon Qualifer (5/9/2015)
Kwenye kampeni zinazoendelea kufuzu Afcon 2017, Tanzania ilicheza vizuri na kuwazidi Nigeria kwa kila kitu kwenye mchezo ule ule.  Farid Mussa, Mbwana Samatta, Ngassa na Ulimwengu walikuwa bora zaidi ya mastaa wa Nigeria.
Bahati mbaya Tanzania haikufanikiwa kufunga bao hata moja na hatimate mechi ikamalizika kwa sare.
  1. Tanzania 0 – 0 Nigeria, International friendly (6 June 1972)
Hii ndio mechi ya kwanza kati ya mataifa haya. Mchezo ulichezwa jijini Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya kutofungana.
  1. Nigeria 2– 0 Tanzania, International friendly (11 September 2002)
Ni miongoni mwa mechi mbili za kirafiki kuwakutanisha Tanzania na Nigeria. Mechi ilichezwa kule jijini Lagos na kuisha kwa Nigeria kupata ushindi.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG