Hatua ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kutoa ratiba ya kufanya
uhakiki wa vyeti vya kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wote
wa umma sasa ni wazi imezidi kupandisha joto kwa vigogo na watumishi
mbalimbali ambao hawana sifa za kielimu kushika nafasi walizo nazo.
Katika taarifa yake ya sasa Baraza la Mitihani nchini, limetangaza
kuwafuata katika maeneo yao ya kazi watumishi wote walioko katika
mamlaka za mikoa, halmashauri na manispaa kwa ajili ya kufanya uhakiki
wa vyeti vyao hivyo vya kitaaluma.