Arsenal walipata bao la uongozi kipindi cha kwanza baada ya beki wa Spurs Kevin Wimmer kujifunga mwenyewe kufuatia mpira mzuri wa adhabu ndogo uliopigwa na Mesut Ozil.
Kipindi cha pili Spurs walikuja vizuri na kufanikiwa kusawazisha bao kwa mkwaju wa penati uliopigwa na Harry Kane baada ya Laurent Koscielny kumfanyia madhambi Mussa Dembele.
Dondoo muhimu
- Arsenal vs Spurs ndiyo mchezo pekee wa Premier League uliozalisha magoli mengi zaidi (139)
- Mauricio Pochettino ni meneja wa kwanza kabisa kuwahi kutokea ambaye hajapoteza katika michezo mitano dhidi ya Arsenal.
- Harry Kane kwa sasa amefikia rekodi ya Gareth Bale kuwa mchezaji wa Spurs aliyefunga magoli mengi zaidi (magoli 5).
- Tottenham hawajafungwa kwenye michezo 11 tangu msimu wa ligi uanze, ikiwa ni mara ya kwanza tangu msimu wa 1960-61.
Tags
MICHEZO KIMATAIFA