
Wafanyakazi wa muda mrefu wa TBL Arusha katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kunukiwa vyeti vya tuzo na motisha
……………………………………………………………………
Kampuni ya TBL Group imewatunukiwa tuzo wafanyakazi wake wa kiwanda cha Arusha waliotumikia kampuni kwa muda mrefu na kwa uadilifu katika vipindi vya kuanzia miaka kumi hadi 35 kwa kuthamini mchango wao walioutoa kwa kampuni.
Hafla ya kukabidhi vyeti vya tuzo vilivyoambatana na zawadi mbalimbali ilifanyika katika kiwanda cha TBL cha Arusha na kuhudhuriwa na wafanyakazi kutoka vitengo mbalimbali vya kiwanda hicho.
Akiongea katika hafla hiyo,Meneja wa kiwanda cha TBL cha Arusha,Salvatory Rweyemamu, aliwapongeza wafanyakazi hao na kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa na kuongeza kuwa kampuni itaendelea kuthamini mchango unaotolewa na wafanyakazi wote unaoiwezesha kuwa kampuni bora kwa kuwapatia motisha mbalimbali

Picha mbalimbali zikionyesha baadhi ya wafanyakazi wa TBL Arusha katika hafla ya kusherehekea mafanikio ya wenzao

Tags
BIASHARA