| Tingatinga la DUWASA likifyeka miwa, mahindi na bustani za mbogambaga zilizolimwa kandokando ya mabwawa ya maji Taka yaliyopo swaswa Manispaa ya Dodoma |
![]() |
| Askari wa kuzuia Ghasia wakiimalisha ulinzi katika eneo hilo |
![]() |
| Wakulima wakiendelea kuvuna nyanya zilizokuwa zikimwagiliwa na maji yaliyotolewa kwenye Bwawa la maji Taka katika eneo la swaswa Dodoma |
![]() |
| wakaulima wakipita katika shamba lililofyekwa miwa na DUWASA ili kupisha hifadhi ya maji taka |
| kazi ikiendelea |
| Tingatinga likiendelea na kazi chini ya ulinzi mkali wa polisi |
Na John
Banda, Dodoma
MAMLAKA ya
maji safi na usafi wa mazingira mjini Dodoma [DUWASA] Imefanya Oparationi ya kuwaondoa
wakulima 88 waliokuwa wakilima Bustani za mbogamboga, mahindi na miwa,
kandokando ya mabwawa ya maji taka yaliyopo Swaswa mjini hapa
Katika Oprationi
hiyo iliyokuwa na ulinzi mkali wa polisi chini ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma
mjini Christina Mdeme magreda na vifaa vingine kama mapanga, makwanja na
majembe yaliyokuwa yakitumiwa na vijana maalumu waliopelekwa rasmi katika zoezi
hilo na DUWASA
Akiongea na
waandishi wa habari wakati zoezi hilo
likiendelea Mkuu huyo wa wilaya alisema utekelezaji huo unafanywa kutokana na
agizo la Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina aliyefika katika eneo hilo hivi karibu
wakati wa ziara maalum na kuagizo wakulima hao waondolewe ili kunusuru afya za wananchi
Mndeme
alisema kitendo cha kulima mazao ya chakula kama mbogamboga, miwa, mahindi na
hata migomba kwa kumwagilia maji machafu kiasi kile ni ukiukwaji mkubwa wa
sheria ya Afya na mazingira hali inoweza kusababisha afya za binadamu kuwa
hatarini
“pamoja na
kuweka doria za mara kwa mara ikiwemo kupanda miti na ukoka katika maeneo yote
yanayozunguka bwawa hili pia nitoe tahadhari kuwa tutamchukulia hatua kali za
kisheria mtu yoyote ambaye atakamatwa akipampu maji hayo machafu kwa ajili ya
kumwagilia bustani”, alisema
Kwa upande
wake Afsa Afya wa manispaa Alecky Barankena alisema mazao hayo ambayo yamekuwa
yakilimwa katika maeneo hayo husababisha athari za magonjwa ya tumbo kama
taiphod, Kipindupindi, minyoo, figo na hata salatani hivyo ili kuzuia hali hiyo
ni kuacha kutumia maji hayo kumwagilia mazao yao
Alisema mwaka
jana katika maeneo yote yanayozunguka eneo hilo za ipagala, kwa mwatano, ilazo
na swaswa yenyewe mwaka jana kulikuwa na mlipuko mkubwa wa kipindupindu na walio
wengi walikuwa wakilima kandokando ya bwawa hilo
Nae Ofsa
mawasiliano wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Sebastian Wariaoba
alisema Oparation hiyo ni ya kuwaondoa wakulima wote waliokuwa katika hifadhi
ya mabwawa hayo ambapo hawakutakiwa kuingia ndani ya mita 100 toka mabwawa
yalipo
Mwenyekiti
wa wakulima hao Elia Yohana alisema wao hawapingani na sheria japo wanajua kuwa
wataathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na wengi wao wanamikopo lakini pia
familia zitakosa kujiendesha kwa kuwa hata hivyo wamekuwa wakifanya kilimo
hicho kwa kipindi cha miaka 36 wao wakiwa 88
Tags
AFYA





