BANDA MEDIA BLOG

MKUTANO MKUU WA UMOJA WA WALIMU WAKUU WAFANYIKA, POR NDALICHAKO AWAKUMBUSHA MAJUKUMU YAO KUSIMAMIA ELIMU, GLOBAL LINK YATOA NENO

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na ufundi Prof, Joyce Ndalichako akisisitiza jambo wakati alipokuwa akifngua mkutano wa umoja wa walimu wakuu wa shule za sekondari uliofnyika mjini Dodoma

Mkurugenzi wa Wakala wa Elimu Nje ya Nchi [Global Education Link] Abdumalik Mollel akifafanua jambo wakati alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa walimu wakuu wa shule za sekondari uliofanyika mjini Dodoma


Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Chrsitina Mndeme akionyesha vodole 4 kama ishara ya magauni 4 kwa wasichana wanaosoma shule ili waweze kuepukana na mimba zisotarajiwa, wakati alipokuwa akitoa salamu za mkoa wa Dodoma kwenye mkutano huo

Rais wa umoja wa walimu wakuu wa shule za sekondari akizungumza katika mkutano huo

Mkurugenzi wa Global Education Link akipokea tuzo ya umahili wa kuchangia Elimu Nchini toka kwa Waziri wa Elimu, sayansi, Teknolojia na ufundi Prof, Joyce Ndalichako [PICHA NA JOHN BANDA]




Walimu wakuu sekondari wakiwa katika ukumbi wa nyerere Dodoma wakati wa mkutano huo




Na John Banda, Dodoma
WAZIRI wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi,Prof.Joyce Ndalichako, amesema Walimu wakuu nchini wanatakiwa amewataka  kusimamia ubora wa elimu kutokana na wao kukaa karibu na wanafunzi.
Akizungumza  jana Mjini hapa wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) Prof.Ndalichako alisema Walimu Wakuu wanawajibu wa kusimamia ubora wa elimu nchini.
Alisema wao ndio wanakaa na wanafunzi hivyo wanawajibu wa kuwa wasimamizi na wakaguzi wa kwanza ili kuiboresha elimu ya Tanzania.
Pia alisema elimu ya Sekondari ni kiungo muhimu katika kuendeleza elimu nchini kwani hapo ndipo wanapotoka wanafunzi wataoenda katika vyuo vikuu na vyuo vya kati.
‘’Serikali itaendelea kuimarisha elimu ya sekondari pia tunaomkakati wa kuimarisha ufundishaji wa masomo ya Sayansi’’alisema Profesa Ndalichako.
Pia alisema kwa sasa utaratibu watakaotumia  kuajiri walimu wa Sayansi kwa sasa umebadilika kwani wale wote waliohitimu Ualimu wa Sayansi na Hisabati wanatakiwa watume vyeti vyao kabla ya kupangiwa kituo cha kazi.
‘’Kwenye Arts tuna walimu wa ziada hao tutajaribu kuwapanga kutokana na shule kwani wengi walikuwa wamepangwa shule moja hivyo tutaangalia utaratibu wa kuwapanga kulingana na mahitaji’’alisema
Pia aliwataka Walimu Wakuu hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa elimu nchini kwani wao ndio wanaowapika wanafunzi kabla ya kwenda vyuoni.
Vilevile aliwataka Wakuu hao kupeleka takwimu sahihi za wanafunzi waliopo katika shule zao ili kuisaidia serikali katika kupanga bajeti ili iweze kutoa fedha sahihi.
‘’Hapa kuna kimbembe wakati mwingine huwa najifanyisha nimepoteza takwimu ya shule fulani nikitumiwa inakuwa tofauti na ile ya mwanzo niwaombe walimu mkalisimamie hili ili iwe rahisi kwetu kupanga bajeti yenye tija’’alisema
Aidha Prof. Ndalichako alisema kutokana na maabara nyingi kukamilkia serikali itatoa vifaa vya maabara kuanzia Januari mwaka huu kwani kwa sasa ndio vimeagizwa.
Kuhusina na mimba wanaopewa wanafunzi,Profesa Ndalichako alisema ni changamoto kubwa kwao na wameunda Kamati ya kushughulikia suala hilo ambayo itampa majibu katika siku za hivi karibuni.
Aidha Waziri huyo alisema Makatibu Tawala na Wakurugunzi kuwalinda walimu wanaofuata kanuni,taratibu na sheria katika utendaji kazi wao likiwemo suala la wanasiasa kuingilia masuala ya elimu.
‘’Wanasiasa wamekuwa wakiingilia suala la elimu niwaombe Wakurugenzi na Makatibu Tawala kulishughulikia suala hilo kwa kuwalinda walimu wakuu ambao wanafuata kanuni,sheria na taratibu’’alisema
Pia aliwataka Walimu wakuu kuwa na mahusiano mazuri na jamii inayowazunguka pamoja na kufanya usafi katika shule zao.
‘’Unafika shule mapaka unajuliza kuna watu wanaishi hapa niwaombe mjitahidi katika suala la usafi ikiwezekana muwe na siku maalum ya kufanya usafi’’alisema
Akisoma risala  Rais wa Tahossa,Bonus Nyimbo aliiomba serikali itoe waraka wa kupiga marufuku  matumizi ya simu kwa wanafunzi mashuleni kwani imekuwa ikichangia kushusha ufaulu wa baadhi ya wanafunzi.
Nyimbo ambaye ni mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Mwenge ya Mkoani Singida aliiomba serikali iajiri walinzi,watumishi na madereva ili waweze kufanya kazi kwa ufasaha.
Alisema changamoto nyingine wanayokabiliwa nayo ni baadhi ya wanachama kutoelewa vizuri katiba pamoja na kutokulipa ada kwa wakati.
‘’Ili kuboresha elimu tunaiomba serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi kwani simu nyingi tunazozikamata tunakuta mule hakuna taaluma’’alisema
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Global Education Link,AbdulMalik Molel ambaye  kampuni yake ilipewa tuzo ya heshima katika kuendeleza elimu nchini,alisema ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiendeleza elimu ya Tanzania.
‘’Kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu,Wazazi,Walezi,Walimu Waambieni wanafunzi wasiwe na ‘Expection’ kwani wakienda vyuo vikuu wanakuwa wasumbufu’’alisema 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG