BANDA MEDIA BLOG

WAZIRI CHARLES MWIJAGE AZINDUA KIWANDA CHA VIUNGO (VEGETA) WILAYANI BAGAMOYO


0001
Mgeni rasmi akiwa waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage wa tatu kushoto,akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kiwanga cha utengenezaji wa viungo,Vegata Podravka Ltd,kilichojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 16,Kushoto ni Mbunge wa jimbo la Bagamoyo,Mh.Shukuru Kawambwa na kulia ni Makamu wa Rais wa Kampuni ya Podravka Group kutoka nchini Croatia,Bi.Olivia Jakupec.
001
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage kikata utepe kwenye cheti cha heshima ya ushiriki wake mkubwa katika uzinduzi wa kiwanda hicho alichokabidhiwa na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Podravka Group kutoka nchini Croatia ,ambayo ni kampuni mama ya Vegeta Tanzania,Bi.Olivia Jakupec  katikati ni  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Vegeta Podravka Ltd-Tanzania  Davor Svar.
01
  Makamu wa Rais wa Kampuni ya Podravka Group kutoka nchini Croatia ,ambayo ni kampuni mama ya Vegeta Tanzania,Bi.Olivia Jakupec akimkabidhi Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage cheti cha heshima ya ushiriki wake mkubwa katika uzinduzi wa kiwanda hicho.Pichani kati ni  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Vegeta Podravka Ltd-Tanzania,Davor Svar.

2
Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Vegeta Podravka Ltd,Bw-Tanzania,.Davor Svar akizungumza kwa ufupi wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho cha viungo mbalimbali,jana mjini Bagamoyo,huku mgeni rasmi akiwa waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage.
 
Davor alisema kuwa wameamua kuwekeza nchini Tanzania kwa sababu imeonekana ni kiungo muhimu katika mambo ya uwekezaji hasa kutokana na eneo lake, miundo mbinu yake,ukuaji wake wa kiuchumi na pia kuwa kiungo muhimu kwa kuwa mwanachama hai wa nchi za Afrika Mashariki na Kati,kufuatia vigezo hivyo,hurahisisha mambo ya kibiashara kufanyika kwa urahisi zaidi.
 
Davor alisema kuwa kufuatia kuanzishwa kwa kiwanda hicho,kimefanikiwa kutoa ajira za kazi zaidi ya 200 katika Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo kazi ya uuzaji na usambaji wa bidhaa za kiwanda hicho.

4
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijagea  akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho wilayani Bagamoyo,Pwani.Waziri Mwijage alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano imeamua kujenga Uchumi wa Viwanda,ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya Watu.
 
“Tanzania sasa tunajenga  viwanda na si Tanzania ya viwanda inawezekana,hiyo ilikuwa kauli mbiu ya zamani,kwa hiyo sasa tunajenga viwanda,mwenye macho haambiwi Tazama”alifafanua Waziri Mwijage.Waziri Mwijage amewashuruku wawekezaji hao kwa kuamua kuja kuwekeza nchini Tanzania,ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais wa awamu ya tano ,Dkt John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Uchumi wa Viwanda unakwenda kwa kasi na kufanikiwa.
5
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Podravka Group kutoka nchini Croatia ,ambayo ni kampuni mama ya Vegeta Tanzania,Bi.Olivia Jakupec akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho cha utengenezaji wa viungo mbalimbali,mjini Bagamoyo mkoani mkoani Pwani.
 
Olivia alisema kuwa wao kama wawekezaji wametembea nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Uganda,Kenya,Burundi,Zambia,Rwanda,Sudani Congo,Afrika Kusini na nyinginezo,lakini wakabaini Tanzania ndio mahali sahihi kwa uwekezaji.”Hivyo tukafanya utafiti,tukabaini eneo la Bagamoyo linafaa kujengwa kiwanda cha aina hiyo,hivyo tukaamua kujenga kiwanda ndani ya mwaka mmoja na nusu,ambacho kimetumia kiasi cha shilingi bilioni 16 mpaka kukamilika.
 
“Tunaishukuru Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,Waziri wa Viwanda Mh.Charles Mwijage,Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na wengineo kwa ujumla, kwa kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji,kiasi kwamba hata nasi tukaiona furasa hiyo na tukachukua hatua ya kuwekeza kiwanda hiki hapa nchini”,alisema Olivia. 
6
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage akiwa pamoja na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Podravka Group kutoka nchini Croatia ,ambayo ni kampuni mama ya Vegeta Tanzania,Bi.Olivia Jakupec kushoto na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Vegeta Podravka Ltd-Tanzania,Davor Svar katikati wakiwa wameketi Meza kuu kulia ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaji Majid Mwanga.
7
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa kiwanda hicho.
8 9
Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha VEGETA wakiwa katika shughuli za uzalishaji wa viungo vya chakula..
10
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage akipata maelezo kutoka kwa watendaji wa kiwansa hicho wakati alipokuwa kitembelea na kukagua uzalishaji.
11
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage akiangalia uzalishaji wa viungo vinavyozalishwa kiwandani hapo.
12 13
Dk Shukuru Kawambwa Mbunge wa jimbo la Bagamoyo katikati akiwa na Teddy Mapunda pamoja na mmoja wa watendaji wa kiwanda cha VEGETA Bagamoyo.
15
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh.Charles Mwijage akitembezwa katika maeneo mbalimbali ya kiwanda hicho.
16
Baadhi ya watendaji wa makmpuni yanayomiliki viwanda vya VEGETA katika nchi mbalimbali.
17
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho.
18 19 20

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG