MWENYEKITI YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA DODOMA MJINI, JABIR SHEKIMWERI AAGIZA STENDI YA DALADALA MAKOLE IANZE KUFANYA KAZI IFIKAPO NOV MOSI MWAKA HUU.
Mweyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Dodoma mjini Jabir Shekimweri akitoa maelekezo ya ukamilishwaji wa zoezi hilo ifikapo mwishoni mwa mwezi huu
Muonekano wa mabanda ya mbao na mirunda ambayo yanatakiwa kuondolewa ili kupisha utanuzi wa stendi ya daladala katika eneo la makole
................................................
NA MWANDISHI WETU, DODOMA
MWENYEKITI wa kamati ya ulinzi na Usalama
Wilaya ya Dodoma mjini Jabir Shekimweri amemuagiza Mkurugenzi wa jiji
hilo Kuhakikisha Stendi na Soko lilipo D' Centre ya Makole kufunguliwa Ifikapo
Nov Mosi Mwaka huu.
Aidha kuhusu kipande cha Ardhi Kilichomegwa katika
sehemu ambayo awali ilitengwa kwa ajili ya kujenga paa kwa ajili ya wauza mbogamboga
na Matunda na kuwaongezea kanisa la Roman Ctholic, amewataka wahusika kusema
kama wamebadilisha ramani.
Akiongea katika D, Centre hiyo ambayo ilitengwa na
Iliyokuwa CDA tangu mwishoni mwa miaka ya 1970 kwa ajili ya Stendi na
Soko la Jamii wakati alipofanya ziara ya kushtukiza amesema Soko Hilo wahusika
wafike kwa ajili ya kukagua Miundombinu iliyopo na kuhakikisha linaanza kazi
mwanzoni mwa mwezi ujao.
"Niombe Afisa Biashara, Jeshi la zimamoto,
LATRA, Afsa Afya Mkiwa Chini ya Afsa Tarafa piteni kukagua na kujiridha
kuhusu Miundombinu hasa ya vyoo na maji ili ifikapo muda huo Stendi I we
imefunguliwa na kuanza kufanya kazi.
Aidha ameuagiza uongozi wa Kata ya Makole
Kuhakikisha Nyumba zote zilizolipwa fidia tangu mwanzoni mwa mwaka huu kuondoa
vitu vyao na waliovamia kujenga vibanda vya mbao kuondoaka ili kupisha eneo
Hilo limwagwe kifusi na kusawazishwa pamoja na kusafishwa kwa ajili kupisha
daladala..
Awali Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa D
Centre, hiyo John Banda amesema kuwa zaidi ya vibanda vya block vimejengwa
katika eneo Hilo kwa Nguvu za wafanyabiashara tangu mwaka 2017 baada ya
kuhamishiwa hapo wakitokea kilipokuwa kituo cha Daladala jamatini na Sarafina
walikovunjiwa
Amesema anaiomba Serikali kutimiza ahidi ya
kuletewa Daladala ili Soko Hilo lifunguke ambapo itachochea mendeleo ya kata
ulipaji wa Kodi na kuliongezea jiji Mapato ambayo yamekuwa yakipotea zaidi
ya Miaka 5 sasa
" Mhe. Mkuu wa Wilaya iwapo jiji wangeweza kutimiza
Hadi hii ya Daladala na tukakubaliana jinsi ya kulipa Kodi mfano hata kwa
20,000 kwa mwezi kila kibanda maana yake jiji kwa mwaka wangekusanya zaidi ya
Bil 1. kwa vibanda Vyote 500 hvyo tunaiomba serikai itusaidia maana baadhi yetu
wamekata mitaji na kuishi maisha ya kubahatisha",
Naye Diwani wa Kata hiyo ya Makole Omary Omary
amesema hao waliojenga vibanda vya mbao na milunda walivamia hivyo
atamuagiza Mwenyekiti wa mtaa huo kuwatangazia ili waondoe vifaa vyao pamoja na
wenye nyumba zilizolipwa fidia kuondoka kwa ajili ya kupisha Mradi huo wa
Serikali uweze kutekelezwa