HIKI HAPA CHANZO CHA MASIMANGO NA MANYASOSO WANAYOFANYIWA WANAUME KATIKA NDOA ...................!!!!
Katikati,ni Mke wa Msaidizi wa Askofu, Mariamu Tabulu, Kushoto ni Mwenyekiti wa Idara ya Wanawake Dayosisi ya Dodoma, Dkt. Juliana Manyerere na Mwenyekiti wa Umoja wa Akina Mama, Kanisa Kukuu la Kati Mkoani Humo Dkt, Tumain Sanga.Mchungaji Samwel Ngajilo wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Dodoma akiwa katika picha ya Pamoja na wanakwaya wa kwaya mbalimbali za kanisa Kuu la mjini Kati
Mwenyekiti wa Idara ya Wanawake Dayosisi ya Dodoma, Dkt. Juliana Manyerere, akizungumza jambo na wanawake anaowaongoza mara baada ya Ibada ya Mwaka mpya wa 2024.
Na John Banda, Dodoma
BANDA MEDIA ONE.COM
IMEBAINIKA kuwa chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika ni
kutokana na watoto wengi wa Kiume kushindwa kujisimamia na kubeba majukumu yao
kama wanaume katika Familia hivyo kugeuka kuwa kama mzigo.
Pia watoto wa kike wamekuwa na nguvu kubwa katika
familia kutokana na Elimu mbalimbali zikiwemo za kujitambua na kujisimamia, walizopewa
kwa miaka kadhaa ya hivi karibuni.
Kutokana na hali hiyo, Idara ya Wanawake ya Kanisa
la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Dodoma imekuja na mkakati katika
mwaka huu wa 2024, wa kuhakikisha inalivalia njuga swala la mtoto wa kiume.
Akiongea na BANDA MEDIA ONE.COM, Mwenyekiti wa
Idara ya wanawake ya kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya
Dodoma Dkt. Juliana Manyerere amesema kwa sasa hali imebadiliaka sana kwani majukumu
mengi ya familia yanabebwa na mwanawake walio wengi.
“mtoto wa
kike amefanyiwa mkakati mkubwa katika jamii ili asionewe, asinyanyaswe,
ajisimamie lakini pia awe na nguvu ya kiuchumi, sasa imefika wakati mtoto wa
kiume aliyekuwa kaachwa kwa muda mrefu amebaki kabweteka katika familia asijue
cha kufanya,
Kibinadamu inapotokea Mwanamke ananguvu ya kiuchumi
analea familia, katika nyumba lazima manyanyaso na masimango yatakuwepo kwa
huyo mwanaume sasa ili ndoa hiyo iweze kusimama inahitaji neema ya Mungu la
sivyo ndiyo maana unaona ndoa nyingi zinavunjika mapema”, amesema
Amesema wao kama idara ya kanisa, katika mikakati
waliyonayo mwaka huu wa 2024, watahakikisha wanatoa Elimu kwa wakristo wa
kanisa hilo na jamii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kumuelimisha mtoto wa kiume
naye aweze kujisimaia na kujua majukumu yake katika familia kutakakochagizwa na
nguvu ya kiuchumi.