DRC cabinet
..................................................................................
..................................................................................
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo, Jean-Michel Sama Lukonde, alijiuzulu jana siku ya Jumanne, na
kusababisha kuvunjwa kwa serikali yake, ofisi ya rais ilisema katika taarifa
yake.
Waziri Mkuu aliwasilisha notisi ya
kujiuzulu kwa Rais Felix Tshisekedi siku nane baada ya kuthibitishwa kwa mamlaka
yake kama naibu wa kitaifa. Sasa atajiunga na bunge kama mjumbe wa bunge hilo.
Lukonde aliteuliwa kuwa waziri mkuu wa
nchi hiyo ya Afrika ya kati yenye utajiri wa madini mnamo Februari 2021.
Alikuwa na umri wa miaka 43 wakati huo.
Baada ya kuchaguliwa tena Desemba,
Tshisekedi alimteua mwakilishi baada ya kuchaguliwa tena Desemba kubainisha
muungano wa walio wengi ndani ya Bunge la Kitaifa kwa lengo la kuunda serikali
yake ijayo.
