BANDA MEDIA BLOG

Wanajeshi 21 watunukiwa nishani ya heshima na Umoja wa Afrika

 



Umoja wa Afrika (AU) umewatunuku nishani ya heshima wanajeshi 21 kwa huduma yao chini ya Ujumbe wa Ufuatiliaji, Uhakiki na Uzingatiaji wa AU (MVCM) ulio katika eneo la Tigray, kaskazini mwa Ethiopia tangu Disemba 2022.

Jukumu lao lilianza baada ya serikali ya Ethiopia na viongozi wa kikundi cha Tigray People's Liberation Front, TPLF kutoka kaskazini mwa nchi waliotia saini makubaliano ya amani Novemba 2022.

Hii ilimaliza vita kati yao vilivyoanza kati ya mwaka 2018 hadi 2020 ambapo watu takriban 600,000 walipoteza maisha, na mamilioni wengine kulazimika kuhama makazi yao.

Wanajeshi 21 walitunukiwa nishani ya heshima katika makao makuu ya Umoja wa Afrika Addis Ababa nchini Ethiopia.

Wanajeshi hao, ni kutoka Ethiopia, Kenya, Nigeria, na Afrika Kusini na walisifiwa kwa kutekeleza majukumu yao kwa kwa bidii, huku wakithibitisha na kuhakikisha uzingatiaji wa utekelezaji wa Makubaliano ya Kudumu ya Kukomesha Uhasama (COHA).

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat alisema wanajeshi wamesaidia "kufikia amani kupitia mchakato ambao umesalia kuwa unaomilikiwa na kuongozwa na Ethiopia tangu kusainiwa kwa Mkataba."

Majukumu yao yalijumuisha kufuatilia mchakato wa upokonyaji silaha, kuwakomboa watu na kuwajumuisha tena katika jamii (DDR), kuwapa makazi wakimbizi wa ndani, kurejesha huduma za kiuchumi na kijamii, kuwezesha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu na ulinzi wa raia katika eneo la Tigray.

"Tuzo munayopokea leo ni shukrani kwa huduma kubwa mulizotoa na mutaendelea kutoa kwa Afrika yetu pendwa na watu wake,” alisema Olusegun Obasanjo, rais wa zamani wa Nigeria, ambaye ni Mwakilishi Mkuu wa AU katika Pembe ya Afrika na Mwenyekiti wa AU kuhusu Mchakato wa Amani wa Ethiopia.

Ethiopia ni nchi ya kwanza kufaidika na Mfuko wa Amani wa AU kwa kupokea dola za Kimarekani milioni 1 kwa ajili ya kusaidia mchakato wake wa upokonyaji silaha, kuwakomboa watu na kuwajumuisha tena katika jamii (DDR).

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG