BANDA MEDIA BLOG

MAOMBI YA KUMUOMBEA RAIS DKT. SAMIA NA WASADIZI WAKE YATIKISA BUNGE LA TANZANIA.

 















                                   ...............................................................................................

NA JOHN BANDA, DODOMA

Viongozi wa  Taasisi ya Kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wasaidizi wake  Aprili 5,2024 wamekutana na kufanya Maombi ya Kuliombea Taifa Bungeni jijini Dodoma.

Akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya Maombi hayo Katibu mkuu wa Taasisi hiyo Dkt. James Lukuba amesema lengo kubwa ni kumuombea Rais na wasaidizi wake ili waweze kutenda haki wanapowatumikia wananchi wanaowaongoza.

“tunalenga taifa letu la Tanzania liwe na amani, liwe na viongozi bora wanaojali maslahi ya wananchi wao wanaowaongoza kwa kuwatendea haki”, amesema

Aidha amesema kongamano hilo ni la pili kuwakutanisha waombaji kupitia jukwaa hilo, ambalo ni mwanzo tu wa kutengeneza njia ya amani kwa watanzania na viongozi wao, amani ni pale wananchi watakapojua thamani ya Nchi yao, amani ni pale watanzania watakapojua thamani ya Viongozi wao na kujua chakufanya ili waweze kuitunza amani iliyopo Tanzania ambayo chanzo chake ni Mungu mwenyewe.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ambaye Pia ndiyo Mmbeba maono Peter Shariff Abubakary  amesema  kazi kubwa ya wajumbe wa taasisi hiyo ambayo inajumuisha viongozi na waumini wa Dini mbalimbali hapa nchi nikuomba tu.

“Jumla ya wanamaombi hawa wapo 5,752 wakipatikana zaidi ya mikoa 22 ya Tanzania huku waliokutana Bungeni Dodoma ni zadi ya 200, kutoka ngazi ya wilaya, mikoa na taifa.”, amesema

Naye katibu Mkuu wa taasisi hiyo Zanzibar Angelina Adam Malembeka amesema wao ni wanajeshi wa Kiroho kwa ajili ya Kuwalinda viongozi Pamoja na wananchi.

“sisi ni wanajeshi wa kiroho, wakati wanajeshi na askari wengine wanalinda viongozi Pamoja na wananchi kupitia sira za moto, sisi ulinzi wetu tnaufanya kiroho kwa njia ya maombi”, amesema

Viongozi wanaenda vizuri, wanafanya vizuri miradi ipo tunaona inatekelezeka, lakini sisi tunawaombea ili kuwatia nguvu, tunahitaji upendo katika jamii na viongozi”, amesema

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG