BANDA MEDIA BLOG

WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA LAJIVUNIA MAFANIKIO HAYA NDANI YA MIAKA 60 YA MUUNGANO

 

 





A JOHN BANDA, DODOMA

               .................................................................................

NA JOHN BANDA, DODOMA

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax Leo Aprili 3, 2024 Ametangaza Mafanikio ya Wizara hiyo iliyoyapta ndani ya miaka 60 ya Muungano Tanzania.

Akitangaza Mafanikio ya Wizara hiyo ambayo ilianzishwa mara baada ya Taifa kupata Uhuru mwaka 1961 huku Waziri wake wa kwanza akiwa Oscar Kambona, mbele ya Waandishi wa Habari Jijini Dodoma Dkt. Tax amesema Nchi inapoadhimisha miaka 60 ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania Wizara ya Ulinzi na JKT ina kila sababu ya kujivunia Mafanikio makubwa iliyoyapata ndani ya vipindi vyote 6 vya uongozi.

Amesema Awamu ya Kwanza ilijenga Nchi, Umoja wa Kitaifa, iliunda Jeshi, Iliindaa Vijana kwa ajili ya Ulinzi wa Nchi yao ambao walimshinda Nduli Iddi Amin Dadaa, mafanikio hayo yakiendelezwa katika Awamu zilizofuata.

Amesema katika Kulinda Mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Uhuru na Usalama wa Nchi, Wizara kupitia JWTZ Imechangia katika kujenga Uchumi Imara ambapo wananchi hujishughulisha na Shughuli za Uzalishaji Mali bila Hofu, Yote yakiwezeshwa na Sera, Sheria, Kanuni na Mipango Madhubuti katika Ulinzi wa Nchi.

Pia Serikali Kupitia Wizara imeendelea kutekeleza na Kuimarisha jeshi kwa Kulipatia Zana na vifaa Bora vya Kisasa, Rasilimali watu na Nyenzo za Sheria ya Ulinzi  wa Taifa (NATIONAL DEFENCE Act (NDA).

Amesema Ili kuimarisha Jeshi Serikali Kupitia Wizara Imeendelea Kuboresha Maslahi kwa Wanajeshi na Watumishi wa UMMA Kadri uwezo wa Kifedha unavyoruhusu, kwa kuwapatia makazi Bora kwa kuwajengea Nyumba, Pamoja na Stahiki mbalimbali, Kuwapandisha Vyeo kulingana na sifa, Vigezo na Taratibu zilizopo.

Aidha Dkt. Tax ameainisha Ujenzi wa makazi bora kwa wanajeshi katika kambi mbalimbali za Jeshi zilizopo kwenye Mikoa ya Arusha, Dae es laam, Dodoma, Kagera, Kigoma, Morogoro, Mwanza, Pemba, Pwani, Rukwa, Tabora na Tanga ambapo Ujenzi wa nyumba hizo umepunguza kwa kiasi kikubwa uhaba wa nyumba Pamoja na changamoto zitokanazo na Wanajeshi kuishi Uraiani.

Ameongeza kuwa Mchango mkubwa wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania katika miaka 60 ya Muungano, ni Ulinzi Madhubuti wa Mipaka yetu, Uhuru na Katiba. “nchi imeendelea kuwa imara na yenye amani katika awamu zote 6”, amesema

Ameyataja mafanikio mengine kuwa ni Pamoja na Wizara kupitia taasisi zake hususani JWTZ, kukabiliana na majanga au maafa kwa kutoa msaada wa uokoaji na ile ya kibinadamu kutokana na taratibu zilizowekwa, ambapo linashirikiana na asasi za kiraia katika miradi ya kimkakati Pamoja na utoaji wa huduma za afya kwa raia wanaoishi katika maeneo ya jirani na kambi za jeshi.

“ takwimu zinaonyesha kuwa Raia wanaopata huduma katika hospitali za jeshi ni asilimia 80”, amesema

Ametanabaisha kuwa Serikali ya awamu ya 6 inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa kipumbelea cha ujenzi wa makao makuu ya Ulinzi wa Taifa ambao unatekelezwa na wataalamu wa ndani ya Nchi kwa Garama ya Serikali “hili ni jambo muhimu ni mafanikio ya kujivunia kwani ni isahara ya uimara wa Taifa letu”, amesema na kuongeza.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG