BANDA MEDIA BLOG

CHUO CHA MIPANGO CHAWAFUNDA WAHADHIRI WAKE KUTUMIA TEHAMA KUFUNDISHIA

 

Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Prof.Provident Dimoso akielekeza jambo wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya mfumo wa kufundishia wa Learning Management System Moodle leo Juni 11,2024 jijini Dodoma

............... 

NA JOHN BANDA, DODOMA

CHUO cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) kimewaita Wahadhiri wake jijini Dodoma kwa ajili ya Kuwafundisha Namna ya kufundisha wanafunzi wake kwa njia ya Tekinolojia.

 Akiongea wakati alipokuwa akiyafungua mafunzo hayo, Makamu Mkuu wa Chuo,Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi wa Chuo cha IRDP Prof.Provident Dimoso amewataka wahadhiri hao kujifunza na kuhakikisha wanauelewa mfumo huo wa Learning Management System Moodle utakaowarahisishia kufundisha. 

Katika mafunzo hayo watakayofundshwa kwa wiki moja yakiwajumuisha Wakuu wa Idara, Maofisa TEHAMA na wale wa maktaba,  Profesa. Dimoso amesema yatakuwa na tija kubwa kwa walimu kwenye ufundishaji lakini pia kwa wanafunzi wenyewe
"Niwaombe mjifunze haya mafunzo vizuri kwa kuuliza maswali mengi na mhakikishe mnaifahamu hii Teknologia ambayo kwa Chuo cha Mipango tunaanza na Moodle,lakini naufahamu zipo Learning System nyingi"amesema.

Aidha Prof.Dimoso ameeleza kuwa Chuo hicho kinaelekea kwenye kutumia Learning Management System ninyi ambao mmepata nafasi ya kujifunza tunatarajia mtauelewa huu mfumo na kwenda kuwafundisha wahadhiri wengine.

Ameongeza kuwa wanafunzi watakaoanza mwaka huu chuoni hapo watatumia mfumo huo na wao wahadhiri watatumia mfumo huo kuwafundisha namna ya kutumia mfumo huo.

Katika hatua nyingine Prof.Dimoso amezitaja baadhi ya faida za mfumo huo wa Learning Management System kuwa ni pamoja na idadi ya wanafunzi kuongezeka ,lakini pia mapato ya Chuo yataongezeka na ubora wa taaluma unaotolewa utaongezeka kwa kutengeneza wataalamu wengi wenye Weledi.

Awali akimkaribisha Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo na Mratibu wa Mafunzo hayo Said Panga ameeleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Elimu ya juu kwa mabadiliko ya Kiuchumi (HEET),hasa katika eneo la kuwajengea uwezo wahadhiri kwa kuwapa mafunzo ya muda mrefu na mfupi.

Aidha kwa upande wa mafunzo ya muda mrefu wahadhiri 5 wemewezeshwa kusoma shahada za uzamivu,
Vile vile mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wahadhiri katika mbinu bunifu za ufundishaji na namna ya kutumia majukwaa ya TEHAMA katika kufundisha na kujifunzia kwa wanafunzi na mfumo huo utawawezesha wahadhiri kufundishia hata wakiwa nje ya eneo la Chuo.

Kwa upande wake Mkufunzi Msaidizi wa Chuo hicho Musa Sadica amesema kuwa kupitia mfumo huo atakuwa popote duniani na kuweza kufundisha bila shida na hata wanafunzi watakuwa wakipakua masomo kwenye mtandao hali itakayowasaidia kusoma kwa urahisi.






Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG