BANDA MEDIA BLOG

KCBL KUWAKUTANISHA WANAHISA WA VYAMA VYA USHIRIKA JIJINI DODOMA JULAI 26,2024

 



                             ........

                   NA JOHN BANDA, DODOMA

MWENYEKITI wa Bodi ya Benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (KCBL) Prof. Gervas Machimu amewaalika wanahisa wa Benki hiyo kuhudhuria kwenye mkutano  mkuu wa 27 unaotarajiwa kufanyika jijini Dodoma hapo kesho julai 26,2024

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Hapa, leo Julai 25,2024 Mwenyekiti huyo amesema kuwa mkutano huo utakaofanyika kesho unalengo la kuwaeleza mafanikio ya utekelezaji na utendaji wa benki hiyo ikiwa ni Pamoja na kufahamu au kujua uelekeo wake katika mwaka unaofuta.

Amesema Benki hiyo imetanua wigo wa kujiendesha kibiashara kwa kugusa miradi mingi ya kimkakati na Kilimo Biashara ikiwemo cha kahawa, korosho, Pamba, na Tumbaku ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Kuwa Waziri wa Kilimo Husein Bhashe.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Banki Hiyo Godfrey Ng’ulah amesema Benki hiyo imefanikiwa katika uendeshaji kimfumo, utawara bora na tija ambapo mkutano huo unatarajiwa kuwa na wajumbe kutoka vyama vikuu vya Vikuu vya Ushirika Union, AMCOS, vyama vya msingi vya Kilimo, Vyama vya akiba na Kukopa, wamiliki hisa  KCBL, wanaushirika na wananchi wa kawada watapata fursa ya kujulishwa namna inavyofanya kazi.

Amesema BENKI YA USHIRIKA YA KILIMANJARO COPARATIVE BANK LIMITED (KCBL) ambayo ilianzia kule Moshi Mkoani Kilimanjaro hivi sasa inaungana mabenki mengine ya Ushirika na kuwa Benki kuu ambayo makao makuu yake yatakuwa jijini Dodoma

Ameongeza kuwa Mkutano huo unatarajiwa kufanyika ukumbini na kwa njia ya Mitandao ya kijamii ambayo itawapa fursa ambao hawatafika kuufuatilia na kutoa maoni yao.

Amesema wajumbe watapata nafasi ya kusomewa Taarifa ya utendaji kazi ya mwaka 2023, safari ya miaka mitatu ya mageuzi ambapo  Benki ya KCBL Pamoja na Benki ya Tandahimba zitaungana na kuwa Benki Kuu ya Ushirika.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG