..................
NA JOHN ISRAEL, NANE- NANE DODOMA
CHAMA kikuu cha Ushirika Mkoani
Kilimanjaro Kikiwezeshwa na Shirika la
Kimataifa la Maendeleo WE EFFECT kimeendelea kupiga kambi katika Viwanja vya
Nane – nane Nzuguni jijini Dodoma kunakofanyika Maonyesho ya Wafugaji na
Wakulima huku kikitamburisha Bidhaa ya Mtindi Lishe
Mtendaji Mkuu wa Chama hicho chenye
Mjumuiko wa Vyama vya Msingi 17 vinavyojihusisha na Ufugaji wa Ng’ombe wa
Maziwa, Erenesti Haule akiongea kwenye Maonyesho ya Nane-nane jijini Dodoma, amesema
katika vyama hivyo wanasindika Bidhaa za Maziwa ambapo yanasindikwa kwa
virutubisho maalumu vinavyosaidia maswala ya kiafya kwa Watoto na wazee.
“tunasindika maziwa salama kwa ajili ya
matumizi ya binadamu, yakitengenezwa na kimea maalumu kwa ajili ya kutibu homa
za matumbo kwa Watoto na wazee”, amesema mtendaji huyo
Aidha amesema soko la maziwa hayo lipo Mkoani Kilimanjaro, na kwamba kama chama wameanza juhudi za kusaka
masoko katika mikoa mingine kwakutumia maonyesho mbalimbali ya Biashara
yakiwemo maonyesho ya Maziwa, maonyesho ya Ushirika na ya Wakulima na Wafugaji
Nane-nane yanayofanyika kitaifa na kikanda ambapo kumekuwa na mwitikio mkubwa.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Chama cha
Mamba kilicho chini ya Dairy Cooperative
Society LTD kinachojishughulisha na Ufugaji Pamoja na ukusanyaji wa maziwa na kisha kuyasindaka, Mercy Mwanga amesema Mtindi lishe aina ya YOBA Halisi na Yoghat wanaitengeneza
kwa usahihi baada ya kupata mafunzo kutoka Shirika la Maendeleo la EFFECT
Amesema kutokana na Kimea hicho kinachowekwa
kwenye Mtindi lishe, kimesababisha faida nyingi za Kiafya zinazotokana na Bidhaa
hiyo ya maziwa inayojulika kwa jina YOBA.
“mtindi lishe huu unaotengenezwa na
kirutubisho maalum unatumika kama chakula, kiburudisho na tiba kwani unashibisha,
pia unatibu vidonda vya tumbo, kuondoa Gesi, unaongeza seli zilizopungua na kuondoa
sumu mwilini”, amesema