NA JOHN BANDA, DODOMA
MWENYEKITI wa chama cha mapinduzi (CCM), Kata ya Iyumbu
jijini Dodoma Sadik Mponyamili amewataka wanachama wa chama hicho kutobweteka
badala yake Waamke wakapige kura bila kujali kutakuwa na mvua au jua siku hiyo.
Sadik ameutoa Wito huo kwenye mkutano wa Kampeni za
chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Mbuyuni Mtaa wa Nyerere, ambapo pia
ametumia nafasi hiyo kumnadi Ayoub Mandabaga anayegombea nafasi ya Mwenyekiti
wa Mtaa huo Pamoja na wajumbe wa serikali ya mtaa.
“ kumekucha tuamke tukapige kura, siku ya uchaguzi
itakuwa ni jumatano ndugu zangu wa mtaa wa Nyerere tuliojiandikisha tukapige
kura kuchagua wagombea wa CCM, bila kujali kutakuwa na mvua au jua siku hiyo
hakuna kulala kama kupanda tukapande alhamis”, amesema
Ayoub Mandabaga Mgombea nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa
wa Nyerere amejivunia, Usambazaji wa Umeme kwa asilimia 100, maji asilimi 80,
ufunguzi wa mtaa kwa miundombinu ya Barabara, kamati ya maafa ambayo kwa sasa
ina vyombo vya kuhudumia kwenye matukio lakini pia kuunda vikundi vya ujasiliamali
kwa ajili ya kuchangamkia fedha za Rais Dkt. Samia Suluhu..
“katika kipindi cha miaka 5 iliyopita najivunia
usambazaji wa maji, umeme, barabara na kamati imara ya maafa naombeni kura zenu
nikaendelee kuwaletea maendeleo wakazi wa mtaa wa Nyerere kwa nina uwezo huo”,
amesema
Awali Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM, Kata ya
Iyumbu Luka Chipanga amewaomba waumini wa Dini mbalimbali, kumwomba Mungu ili
kusitokee umauti kwa mpiga kura yoyote katika kata hiyo kabla ya siku ya
uchaguzi na kwamba ili ujenzi wowote uwe Madhubuti lazima ufanyike hatua kwa
hatua hivyo wagombea hao wapewe kura ili wakaendeleze walipoishia.
Mwenezi wa CCM, Kata ya Iyumbu akifurahia jambo wakati alipokuwa akizungumza na wanaccm kwenye mkutano huo wa kampeni
Elias Sutuchi (KING), Diwani wa kata ya Iyumbu akiongea jambo kwenye mkutano huo wa kampeni kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa.