NA JOHN BANDA, DODOMA
Mwenyekiti wa mtaa wa chinyoyo kata ya kilimani
jijini Dodoma Faustina Bendera amewaonya wananchi kuacha tabia ya kukusanya na
kusomba mchanga pebezoni mwa barabara za mtaa huo la sivyo watachukuliwa hatua
kali ikiwemo kufikishwa mahakamai
Bendera ametoa onyo hilo baada ya kuona
baadhi ya wanachi wakichota mchanga baada ya mvua kuanza kunyesha hivi karibuni,
huku wakisababisha uharibiu wa miundombinu ya barabara hizo.
"Hivi karibuni baada ya mvua
kunyesha kuna wananchi wameanza tabia ya kukusanya malundo ya mchanga katika
barabara za mtaa Sasa ninawaambia ni marufuku kumwona mwananchi yoyote akisomba
mchanga katika barabara za mtaa na yoyote tutakaye mkamata na kumchukulia hatua
kali za kisheria ikiwa kupigwa fani na kupelekwa mahakamani"amesema
Mwenyekiti Faustina
Aidha Mwenyekiti huyo amesema wanaotaka
kusomba mchanga waende kwenye mtaro mkubwa unaujulikana kama mtaro wa wizara ya
afya kwakuwa kuna mchanga unaoletwa na maji ya mvua pia watakuwa wamesaidia
kuusafisha mtaro huo.
Mbalimbali na hilo mwenyekiti Faustina
amewataadharisha wananchi katika kipindi hichi cha masika kuhakikisha wanafanya
usafi katika maeneo yao ya nyumbani na mtaani ili kuhakikisha wanaepukana na
magonjwa ya kuharisha (kipindupindu) ambacho kwa tarifa zilizopita tayari
kimeshabisha hodi jijini Dodoma naekusababiaha vifo.
Aidha Mwenyekiti huyo amewasisitiza
wananchi kuhakikisha wanatunza miundombinu ya barabara zote za mtaa na kuwa
wanatoa taarifa za maafa yoyote yatakayokuwa yanatokana na mvua hizi
zinazoendelea kunyesha hapa Jiji Dodoma.
