BANDA MEDIA BLOG

ANDIKO LA ALI KAMWE BAADA YA YANGA KUFUNGWA NA DODOMA JIJI


Hii imeshaisha Wananchi. Kila mtu ana siku mbaya kazini. Prince Dube na Mwamnyeto tunaosikitika nao leo ndio waliotupa furaha sana kwenye Derby.

It’s Football. Malengo yetu hayakuwa kumaliza msimu bila kufungwa, Malengo ni UBINGWA. Tumeteleza leo lakini Alhamdulillah bado Ubingwa uko kwenye mikono yetu

Ni sisi kuamua, tuweke vichwa chini na kuendelea kuwachambua Players wetu Au tulibebe hili kwa kushukuru Tuendelee na uwanja wa mapambano

Tusicheze midundo ya wanafki wanaotuombea mabaya kila leo. Wao Yanga ikishinda, Ligi mbovu. Yanga ikifungwa, Usajili mbovu. 

Niliposimama na kusema kuwa, Ligi ni ngumu na tunapaswa kuiheshimu Yanga inaposhinda nilimaanisha Football kwa kiwango kikubwa sana

Bado mechi 7 wanangu.. Tuna Faida ya pointi kileleni na sina mashaka kabisa, Tukisimama pamoja, Tutafanya vizuri In Shaa Allah

Daima Mbele Nyuma Mwiko🔰👊🏼

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG