Hii imeshaisha Wananchi. Kila mtu ana siku mbaya kazini. Prince Dube na Mwamnyeto tunaosikitika nao leo ndio waliotupa furaha sana kwenye Derby.
It’s Football. Malengo yetu hayakuwa kumaliza msimu bila kufungwa, Malengo ni UBINGWA. Tumeteleza leo lakini Alhamdulillah bado Ubingwa uko kwenye mikono yetu
Ni sisi kuamua, tuweke vichwa chini na kuendelea kuwachambua Players wetu Au tulibebe hili kwa kushukuru Tuendelee na uwanja wa mapambano
Tusicheze midundo ya wanafki wanaotuombea mabaya kila leo. Wao Yanga ikishinda, Ligi mbovu. Yanga ikifungwa, Usajili mbovu.
Niliposimama na kusema kuwa, Ligi ni ngumu na tunapaswa kuiheshimu Yanga inaposhinda nilimaanisha Football kwa kiwango kikubwa sana
Bado mechi 7 wanangu.. Tuna Faida ya pointi kileleni na sina mashaka kabisa, Tukisimama pamoja, Tutafanya vizuri In Shaa Allah
Daima Mbele Nyuma Mwiko🔰👊🏼
