Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatazamiwa hii leo kuidhinisha
kwa kauli moja azimio lililoandaliwa na Ufaransa linalonuia kuhitimisha
mgogoro wa kisiasa nchini Burundi. Iwapo azimio hilo litapasishwa, basi
Umoja wa Mataifa utaanzisha mchakato wa kutuma vikosi vya kulinda amani
katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Kadhalika azimio hilo
linapendekeza kuwekewa vikwazo shakhsia wa kisiasa wanaochechea
machafuko nchini humo. Duru za kidiplomasia za Ufaransa zimeeleza
matumaini yao kuwa azimio hilo litaungwa mkono na wananchama wote 15 wa
Baraza la Usalama. Zaidi ya watu 240 wameuawa huku wengine zaidi ya laki
2 wakilazimika kuitoroka nchi na kuwa wakimbizi katika nchi jirani,
tangu machafuko yaanze nchi Burundi mwezi Aprili mwaka huu. Machafuko
hayo yalianza baada ya Rais Pierre Nkurunzinza kutangaza azma yake ya
kuwania urais kwa muhula wa tatu, hatua ambayo wapinzani nchini humo
wanashikilia kuwa ilikiuka katiba ya nchi.
Tags
KIMATAIFA