BANDA MEDIA BLOG

DIWANI MAGUWO AKABIDHIWA CHETI, AMTAKA MAGUFULI CHAMWINO.



Diwani mteule wa Kata ya Chamwino Ikulu Julius Maguwo (kulia)akipokea cheti cha ushindi kutoka kwa afisa mtendaji wa Kata hiyo,Adrego Asanga (kushoto)jana katika ofisi za afisa Mtendaji wa Kata hiyo. Picha na Ramadhan Hassan

Na John Banda,CHAMWINO
DIWANI Mteule wa Kata ya Chamwino Ikulu,Julius Maguwo(CCM) amemkaribisha Rais mteule Dk John Magufuli katika ikulu ya Chamwino Dodoma kwa ajili ya mapumziko kutokana na hekaheka za uchaguzi.

Diwani mteule wa Kata ya Chamwino Ikulu (CCM)Julius Maguwo akionesha cheti cha ushindi mara baada ya kukabidhiwa jana katika ofisi ya afisa Mtendaji.
 Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi na Msimamizi wa uchaguzi katika Kata hiyo,Asanga Adrego,Maguwo alisema pamoja na kuchaguliwa ni jukumu lake kuhakikisha Rais anakuwa katika mikono salama kutokana na eneo lake kuwa Ikulu.

‘’Hapa ni Ikulu hivyo kutokana na mikimiki ya uchaguzi namwomba Dk Magufuli aje apumzike namwaahidi atakuwa sehemu salama na yenye utulivu,kwani hata Mwalimu Nyerere,Jakaya Kikwete na Benjamini Mkapa wameitumia sana hii Ikulu’’ 

 Pia Maguwo aliahidi kutekeleza kwa viendo ahadi yake aliyoihaidi ya kuhakikisha Kata hiyo inakuwa na maji safi na salama katika kipindi chake ambacho atakuwa madarakani.
Maguwo alisema pia atahakikisha katika Kata hiyo madawati yanapatikana katika shule pamoja na kuzitatua changamoto zote zinazohusu maendeleo.

‘’Yale yote nilioahidi nitatimiza nitayatekeleza kwa kushirikiana na ninyi nia yetu ni kuwa Ikulu inakuwa na hadhi pamoja na kuzitatua kwa wakati changamoto zilizopo’’alisema

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG