Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP David A. Misime atoa ufafanuzi baada ya kutokea
taharuki, maswali mengi na kuenea kwa uvumi mwingi kuwa KABURU RAMADHAN, mwenye
Ualbino ameuwawa na watu wasiojulikana katika mtaa wa Mwausi Kata ya Majengo
Wilaya ya Dodoma.
| Askari Polisi wakiufanyia uchunguzi mwili wa Albono aliyekutwa kafa katika Mjengo Dodoma |
Katika
taarifa yake Kamanda Misime alisema; Leo tarehe 09.01.2016 majira ya saa 07:00
asubuhi tulipokea taarifa kuwa huko katika Mtaa wa Mwausi, Kata ya Majengo,
Wilaya ya Dodoma kuna mtu mwenye Ualibino anaonekana ameuawa.
Baada
ya kupokea taarifa hiyo nilifika katika eneo la tukio nikiwa na Afisa Upelelezi
wa Mkoa na Wilaya pamoja na Wataalam wa Ukaguzi wa matukio ya kijinai.
Tulikuta
mwili wa mwanaume mwenye ualibino na pembeni yake kukiwa na damu.
Baada
ya Uchunguzi wetu wa awali wa kitaalam tuligundua mwili wake haukuwa na jeraha
lolote lile na hana upungufu wa kiungo chochote. Kulingana na uchunguzi huo wa
awali ambao tulishirikisha baadhi ya wana ndugu tulibaini damu iliyookuwa
ikionekana ni matapishi yaliyochanganyikana na damu.
Mtu
huyo kwa mujibu wa ndugu zake anaitwa KABURU S/O RAMADHANI, MIAKA 32,
MNYAKYUSA, MKAZI WA KIKUYU KWA MAKBEL.
Ili
Kujiridhisha zaidi na chanzo cha kifo chake mwili ulifanyiwa uchunguzi na
Daktari na kutoa maoni yake ya kitaalam kuwa kifo chake kimechangiwa na mambo
matatu:-
1. VIDONDA VYA TUMBO –
ambavyo vimeota usugu na kusababisha kuvuja kwa damu ndani ya tumbo (UPPER G1
BLEEDING)
2. KUKOSA MAJI MWILINI –
ambako kumesababishwa na kutapika kwa muda mrefu bila kupata msaada wa maji
(HYPOVOLAEMIC SHOCK)
3. KUKOSA HEWA:
hii imetokana na kutapika akiwa amelala chali na kusababisha matapishi kuziba
njia ya hewa.
Hivyo
basi kwa mujibu wa Uchunguzi wa awali wa Polisi na wa Daktari ambaye kwa mujibu
wa Sheria ndiye mwenye mamlaka ya kutoa maoni ya kitaalam nini chanzo cha kifo
cha marehemu, kifo hicho hakikutokana na Mauaji kama ilivyoripotiwa awali au na
uvumi unaoenezwa mitaani bali ni kifo cha kawaida kilichotokana na sababu
nilizozieleza hapo awali.
Wito
kwa wananchi wanapohisi ugonjwa wowote waende Hospitali ili wapate ushauri wa
kitaalam utakaosaidia kupata tiba. Watu wasinywe pombe bila kula na kupita
kiasi. Mwisho waepuke kusambaza taarifa ambazo hazijathibitishwa na wataalam.
Imetolewa
na
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma
(Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Polisi - David Misime)
Tags
HABARI KITAIFA