masanduku ya miili ya marehemu waliopoteza maisha kutokana na mafuriko Kibaigwa kabla ya kuagwa wilayani Kongwa Dodoma mapema leo Jan 5,2016
BANDA BLOG, Kibaigwa.
MAELFU ya wakazi wa Manispaa ya Dodoma Watumishi wa jeshi la polisi wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa
jana aliwaongoza kuaga miili ya
marehemu wanne wa familia moja akiwemo msaidizi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini Gerald Ryoba.
Ryoba akiwa na familia yake akiwemo
dereva wake na mfanyakazi wake wa ndani walifariki katika ajali ya gari mjini
Kibaigwa baada ya gari lao kusombwa na maji katika eneo la Bwawani.
Akizungumza wakati wa kuiaga miili hiyo
katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma Mkuu huyo wa Mkoa alisema vifo
hivyo vimeushtua uongozi na wananchi wa
Mkoa wa Dodoma na Taifa kwa ujumla kwani kupoteza familia yote kwa wakati mmoja si jambo la
kawaida.
Gallawa aliwataka Wananchi na
Wafanyakazi wa Jeshi la Polisi wanatakiwa kuwa watulivu katika kipindi hichi
kigumu huku akiwataka kuwaomba kwa Mwenyezimu ili awapokee kwa amani.
‘’Niwape
pole wafanyakazi wa Jeshi la Polisi pamoja na Watanzania kwa kuondokewa na hawa
ndugu zetu,tunatakiwa kuwaombea ili mungu awapokee kwa amani’’alisema Gallawa
kwa majonzi.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoani
hapa,David Misime alisema mara baada ya kuiga miili hiyo Ryoba na familia yake
watasafirishwa kuelekea Mkoani Geita.
Kamanda Misime alisema Koplo Ramadhan
atasafirishwa kwenda Lindi huku Sara akipelekwa kwao Mbinga Mkoani Ruvuma kwa
ajili ya mazishi.
‘’Mara baada ya kumaliza kuaga
tutaisafirisha miili kulingana na mahali inapotoka’’alisema
Kwa mujibu wa kamanda huyo alisema juzi Ryoba na
familia yake walikuwa wakitokea mkoani Geita kuelekea Dar es salaam kwenye gari
lenye namba za usajili T 516 DEP aina ya RAV 4 ilokuwa na jumla ya abiria sita.
Alisema marehemu waliokuwepo katika
gari hilo kuwa ni Gerald Ryoba ambaye ni msaidizi wa Mkuu wa jeshi la Polisi
nchini, watoto ambao ni Gabriel Gerald Ryoba, Godwin Gerald Ryoba na mkewe
Fidea John Kiondo.
Wengine ni Dereva wa gari hilo
F.3243 Koplo Ramadhan, Msichana wa kazi aliyefahamika kwa jina la Sara
mwenyeji wa mbinga Mkoani Ruvuma.
Akifafanua kuhusu tukio hilo, Misime
alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa tatu usiku katika eneo la
kibaigwa linalojulikana kwa jina la bwawani wilayani Kongwa.
Alisema polisi walipata taarifa kuwa
kuna maji mengi yanapita katika eneo hilo na yamesababisha magari kushindwa
kupita.
Alisema maji hayo yalikuwa yakitiririka
kutoka maeneo ya Njoge na Hembahemba na baada ya kufika eneo la tukio
walipata taarifa kuwa kuna gari imesombwa na maji hayo.
“Lakini baadaye tulipokea taarifa
kuwa kuna gari imesombwa na maji lakini inaonekana matairi yapo juu, tulianza
kufuatilia na tukazuia magari kuanza kupita na baada ya maji kupungua ndio
tukaruhusu magari kupita,”alisema Misime
Aidha alibainisha walianza hekaheka za
kutafuta gari hilo na baadaye usiku wa manane walifanikiwa kuipata na baada ya
kuitoa kwenye maji walikuta miili ya watu wawili.
“Baada ya kukata lile gari maana
lilikuwa limepondeka tukafanikiwa kutoa mwili wa Fidea John Kiondo ambaye ni
mwalimu wa manispaa ya Temeke ambaye ni mke wa mkaguzi wa polisi Gerald Ryoba
ambaye ni msaidizi wa Afande IGP,”alisema Kamanda huyo.
Hata hivyo alisema walipata taarifa
kuwa katika gari hilo kulikuwa na watu sita na ndipo wakaendelea na harakati za
kutafuta miili mingine.
“Baadae tulifanikiwa kupata mwili wa
dereva wa gari hilo ambaye ni F.3243 Koplo Ramadhan ambaye naye alifariki
na tukaendelea kutafuta na baadaye tukapata mtoto wa miaka minne Gabriel Gerald
Ryoba na hatimaye tukapata mwili wa Godwin Gerald Ryoba,”alisema Misime.
Hata hivyo alisema Mwili wa Mkaguzi
huyo ulipatikana jana saa 10:20 asubuhi na pia katika gari hilo kulikuwa na
Msichana wa kazi aliyefahamika kwa jina la Sara.
mwisho
Tags
HABARI KITAIFA

