BANDA MEDIA BLOG

Naibu Waziri wa Habari Mh. Anastazia Wambura akutana na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh.Said Meck Sadiki

mek1
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura (kulia) akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh.Said Meck Sadiki wakati wa ziara ya Mh. Naibu Waziri aliyoifanya katika Wilaya ya Temeke kukagua viwanja vya wazi vilivyokusudiwa kwa ajili ya michezo ambavyo vimemiwa na baadhi ya wananchi.(Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).
mek2
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura (kulia) akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh.Said Meck Sadiki wakati wa ziara ya Mh. Naibu Waziri aliyoifanya katika Wilaya ya Temeke kukagua viwanja vya wazi vilivyokusudiwa kwa ajili ya michezo ambavyo vimevamiwa na baadhi ya wananchi.(Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).
mek3
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura (kulia) akiagana na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh.Said Meck Sadiki tayari kuanza ziara ya kukagua viwanja vya wazi vilivyokusudiwa kwa ajili ya michezo vilivyovamiwa na baadhi ya wananchi.(Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).

mek4
Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Mainispaa ya Temeke Bw.Waziri Kombo akimkabidhi Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura  taarifa ya utekelezaji kuhusiana na shughuli za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo za Halmashauri hiyo, kulia ni Mbunge wa jimbo la Temeke Mh.Abdalah Mtolea na kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mh.Salum Fesal. (Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).
mek5
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura wa pili kutoka kulia akikagua Uwanja wa Tandika ambao una mgogoro na wapangaji wa maduka ambapo aliagiza siku saba kwa wavamizi wote nchini kutoka kwenye viwanja hivyo kwa ajili ya kupisha shughuli za michezo, wa pili kutoka kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mh.Salum Fesal. (Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).
mek6
Mwenyekiti wa Bodi ya Mikono Arts aliyesimama Bw.Henry Clemensi  akiongea na Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura kuhusu shughuli wanazofanya ili kuwasaidia wasanii wa sanaa za uchongaji ikiwa ni pamoja na kuwatafutia soko nje ya nchi, wa kwanza kulia waliokaa ni Mbunge wa jimbo la Temeke Mh.Abdalah Mtolea na wa kwanza kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Mh.Salum Fesal. (Picha na Benjamin Sawe-WHUSM).

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG