BANDA MEDIA BLOG

CHINA KUJENGA MJI WA KISASA DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana akiteta jambo na Balozi wa China Dkt, LU Youqing.


MKUU wa Mkoa wa Dodoma  Jordan Rugimbana mwishoni mwa wiki amekutana na Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing na kuzungumzia masuala ya kukuza uwekezaji na ushirikiano baina ya pande hizo mbili.
Rugimbana amemwelezea Balozi huyo ofisini kwake mjini Dodoma kuwa ameunda kikosi kazi cha Masuala ya Uwekezaji ambacho kina kazi ya kuboresha mazingira ya uwekezaji, kutambua wawekezaji waliopo na changamoto zinazowakabili na njia bora za kuzitatua kwa lengo la kuboresha mazingira na kukuza uwekezaji Mkoani humo.

Amesema kwa sasa anataka kuanzisha eneo maalum la uwekezaji kwenye Mkoa wa Dodoma ambapo kitaundwa kituo chenye kutoa huduma zote zinazohitajika kwenye uwekezaji na kutakuwa na taasisi zote zinazohusika na utoaji wa huduma hizo ambapo mwekezaji akifika kituoni hapo hana haja ya kuondoka kwenda kutafuta huduma sehemu nyingine, mahitaji yake yote yatatatuliwa hapohapo kituoni na mara moja ataanza shughuli yake ya uwekezaji.
Balozi wa China Nchini Dkt, Lu Youqing akiwa na ujumbe wake walipotembelea ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dodoma
Pamoja na masuala hayo ya uwekezaji, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alimshirikisha Balozi wa China juu ya mpango wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa mji mpya wa serikali hapa mkoani humo wenye lengo la kukamilisha ujenzi wa miundombinu yote muhimu na kuhakikisha serikali inahamia Makao Makuu Dodoma.
RUGIMBANA NA DKT, LU
Kwa upande wake Balozi Dkt. Lu Youqing alimshukuru Mkuu wa Mkoa Dodoma kwa jinsi ambavyo uongozi wake wa Mkoa ulivyoweka utaratibu wa makusudi wa kuboresha mazingira ya uwekezaji na kuanza kushughulikia changamoto zinazowakabili wawekezaji kwa kushirikiana nao na kusema kuwa anapata taarifa nyingi kutoka kwa wawekezaji wa kichina wanaoendesha shughuli mbalimbali Mkoani Dodoma juu ya namna ambavyo uongozi wa Mkoa unashirikiana na wawekezaji hao kutatua changamoto zilizopo.
Vilevile, Balozi wa China alimhakikishia Rugimbana kuwa  atasaidia kuzikutanisha Mamlaka zinazoshughulikia ujenzi wa mji mpya wa serikali na serikali kuhamia Dodoma na mamlaka ya Manispaa ya Jiji la Beijing China ambayo inauzoefu na imefanikiwa kujenga mji mpya mbali na ule wa zamani kwa kipindi cha miaka miwili tu, lengo likiwa kubadilishana uzoefu katika kutekeleza mradi huo wenye manufaa makubwa kiuchumi hapa Tanzania.


Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG