Hapa
ni katika Msikiti wa Masjid Latif Ahmadiyya Muslim Jamaat Nsalala
uliopo kijiji cha Nsalala ,kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga ambapo leo
Jumapili Mei 22,2016 Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Mkoa wa
Shinyanga(Ahmadiyya Muslim Jamaat Shinyanga) imefanya mkutano wa Mwaka
wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Shinyanga ukiwa na kauli mbiu ya ” Love For All
Hatred For None (Mapenzi Kwa Wote Bila Chuki Kwa Yeyote”.
….
Mgeni
rasmi alikuwa katibu tawala msaidizi idara ya uchumi na uzalishaji
aliyemwakilisha kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga John Mongella huku
waumini wa dini hiyo kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga
wakihudhuria mkutano huo.
Mkutano
huo uliolenga kuhamasisha amani katika jamii kwa kuwakumbusha waumini
kumjua mwenyezi mungu hali itakayosaidia kupunguza hata kumaliza kabisa
vitendo vya kihalifu ikiwemo mauaji ya watu wasio na hatia kama vile
vikongwe na albino, umehudhuriwa pia na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya
Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry
(pichani juu).
Akizungumza
katika mkutano huo Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania
Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry alieleza kusikitishwa na kitendo
cha mauaji ya watu watu msikitini na kuongeza kuwa dini ya kiislam
hairuhusu vitendo kama hivyo huku akiviomba vyombo vya dola kufanya
uchunguzi ili kubaini wahusika wa kitendo hicho haramu.
Kupitia
mkutano huo jamii imeelimishwa juu ya dhana potofu dhidi ya uislamu
ambapo baadhi ya watu wamekuwa wakihusisha dini hiyo pamoja na vikundi
vya kigaidi mfano wa Boko haram, Isis, Al-shabaab na vingine vingi
ambavyo vimekuwa vikidhuru binadamu.
Mada
mbalimbali zimetolewa na viongozi wa jumuiya hiyo ikiwemo nafasi ya
dini katika maisha ya binadamu,malezi ya watoto na majukumu ya wazazi
sawa na mafundisho ya dini ya kiislamu,umuhimu wa kuwa kiongozi
(Khalifa) wa kiroho na barakaza ukhalifa pamoja na masharti ya kujiunga
na jumuiya hiyo(masharti 10 ya Baiat na wajibu wa waumini.
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa mkutano huo,ametusogezea picha 55 kilichojiri..
Hapa
ndipo Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Mkoa wa Shinyanga
waumini wa dini ya kiislamu kutoka Jumuiya hiyo kutoka ndani na nje ya
mkoa wa Shinyanga wamejitokeza kwa wingi kusikiliza mawaidha mbalimbali
kutoka kwa viongozi wa Jumuiya hiyo pamoja na wageni waalikwa akiwemo
kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mohammed Idd Nchira
Bango likionesha kilichokuwa kinaendelea
Katibu
Mkuu Msaidizi wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya nchini Tanzania
Abdulrahman Mohammed Ame akitoa mada kuhusu Haja ya nafasi ya dini
katika maisha ya binadamu ambapo alitumia fursa hiyo kuitaka jamii
kutenda mambo mema na kujiepusha na vitendo vya kihalifu ikiwemo kuua
watu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.
Alisisitiza
kuwa uislamu ni dini ya amani hivyo kuwataka binadamu kuishi kwa amani
na kwamba kitendo cha kuua mtu mmoja ni sawa na kuua dunia nzima.Hata
Hivyo Ame alisema sera ya jumuiya hiyo ni kutochanganya siasa na dini .
Meza
kuu,wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya
Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry,kushoto kwake ni mgeni
rasmi Mohammed Idd Nchira,akifuatiwa na rais wa Jumuiya hiyo Kanda ya
Ziwa Salim Thani,wa kwanza kushoto ni Naibu rais wa jumuiya hiyo Kanda
ya ziwa Yahaya Kamba Ulaya.Wa kwanza kulia ni Mbashiri wa kanda ya ziwa
wa jumuiya hiyo Sheikh Waseem Khan
Waumini wa dini ya Kiislam kutoka maeneo ya mjini na Vijijini ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga waliojitokeza katika mkutano huo
Mgeni rasmi katika mkutano huo Mohammed Idd Nchira akiwahutubia waumini wa dini ya kiislamu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya.
Tags
HABARI ZA DINI