BANDA MEDIA BLOG

Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanakuwa na miundombinu iliyobora-Profesa Mbarawa

p1Na Betrice Lyimo-MAELEZO
…………………………………
Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya   Mabey  Bridge   ya nchini  Uingereza wamejipanga kikamilifu kujenga  barabara tatu za juu (Fly Overs) na  barabara nne   za watembea  kwa lengo la kupunguza  msongamano wa  foleni jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa leo na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa  Makame Mbarawa wakati wa   mazungumzo hayo na  kampuni ya   Mabey  Bridge  ya Uingereza  kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo nchini.
Profesa Mbarawa  alisema kuwa barabara hizo  zitajengwa  hasa maeneo ambayo yana msongamano  mkubwa  wa magari  ikiwa  ni pamoja na  eneo la barabara ya Mwenge.
“Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha  wananchi  wanakuwa na miundombinu iliyobora  hasa katika  upande wa  barabara za magari na barabara za waenda kwa miguu ili kuwarahisishia wananchi  kuwahi kuwajibika katika maeneo yao ya kazi”.
Mbali na hayo,  Waziri Mbarawa alifanya ziara ya kushtukiza  katika Daraja la  Nyerere lililopo maeneo ya   Kigamboni kwa  lengo la kutaka kujua maendeleo ya daraja hilo na  kumtaka msimamizi wa  daraja hilo kuandaa   kadi maalumu  au kitambulisho  zitakazotumika kwa lengo la  kupunguza msongamano  wakati wa kulipia tozo.
vilevile Waziri aliwataka  wananchi  kuwa waangalifu na miundombinu ya   daraja hilo  na  endapo  kuna mtu  atakaye bainika  kuharibu   atachukuliwa  hatua kali za kisheria ikiwa  ni pamoja  na  kulipa faini za gharama ya juu.
“kuanzia sasa  kunatakiwa kuwepo na  faini kali  kwa mtu yeyote atakaye haribu  miundombinu ya daraja  hili kwa lengo la kulifanya daraja   lidumi kwa muda mrefu” alisisitiza Waziri Mbarawa
Kwa upande wake  Msimamizi   Mkuu  wa daraja la Nyerere, Gerald  Sondo  alisema   wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya madereva wa  daladala kushindwa kutumia daraja hilo na  kudai kuwa tozo ni kubwa.
 Vilevile  Waziri huyo alifanya ziara  katika eneo la ujenzi wa  mtambo wa Mafuta kutoka kwenye meli kabla ya kuingia kwenye matanki (Flow Meter)  kuona maendeleo ya ukarabati wa mtambo hio uliyoharibika hivi karibuni  kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali   na   kumtaka mkandarasi  kuhakikisha  eneo hilo linazungishiwa   ukuta  ili kuziba  mitambo  hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG