BANDA MEDIA BLOG

MERCY KITOMARI, MJASIRIAMALI KIJANA ANAYETAKA KUMUONA ‘ROLE MODEL’ WAKE RAIS MAGUFULI


Mjasiriamali kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari wakati akizungumza na Meneja Uendeshaji wa mtandao wa Habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige (hayupo pichani).
…………………………………………………………………………..

MJASIRIAMALI kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari amesema anatamani kukutana na Rais John Pombe Magufuli kumwelezea haja ya kukutana na wanawake wajasiriamali vijana wamweleze matatizo yao.
Amesema Rais baada ya kukutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara , inafaa akutane na wajasiriamali wanawake vijana ambao wanapita katika magumu mbalimbali .
Alisema katika mahojiano hivi karibuni ambayo sehemu yake itachapishwa katika mtandao wa Modewjiblog muda wowote kwamba, rais Magufuli akiwa kama ‘Role Model wake’ katika kujituma, anaweza kuwasikiliza wanawake hao vijana na kusaidia kuwasukuma juu zaidi katika kampeni ya kuiweka Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
“Nimekuwa nikikutana na wanawake wenzangu ambao wamekata tamaa na wamekuwa wakiniuliza ninawezaje kuendelea, nikawambia wasi-give up (wasikate tama) na kwamba serikali hii ni ya viwanda na kuchapa kazi “ alisema na kufafanua kwamba wanachohitaji wanawake hao ni mazingira mazuri ya kufanya ujasiriamali.
Mercy ambaye anatengeneza ‘ice cream’ zinazotumia matunda yote ya kitanzania kama vile fenesi, nanasi, bungo, ndizi, embe ana ndoto ya kumiliki kiwanda kikubwa kinachoweza kutengeneza na kufikisha ashkrimu kwa Tanzania na Afrika Mashariki ifikapo mwaka 2020.
Akiwa ameanza kazi hiyo mwaka 2010 kutoka ‘jiko’ la nyumbani Mercy amefanikiwa kutambua wigo wake wa biashara ambayo amesema ina changamoto nyingi hasa mifumo ya vibali na ulipaji kodi na ushuru.

Muonekano wa nje wa duka la Ice Cream la Nelwa’s Gelato lililopo ndani ya Petrol Station ya SOPCO barabara ya Morogoro-Magomeni Mwembechai karibu na kwa Sheikh Yahya.
Alisema uwapo wa kodi nyingi zenye viwango sawa kati ya anayeanza na aliyekuwepo; anayeingiza kidogo na kikubwa kunaleta athari kubwa kwa wajasiriamali wanaotaka kuchomoza.
“To be honest (nikiwa mkweli) zinavunja moyo… nyingi zinakwamisha kwani sisi waelewe tu kwamba tunatengeneza ajira na tunatengeneza soko kama mimi nanunua matunda natengeneza soko la mkulima.,.. natengeneza ashkrimu (Ice Cream) natengeneza ajira.. ipo haja ya kuangalia mambo mengi na hasa hili la kodi na ushuru” alisema.
Alisema ana mambo mengi ya kumwambia Rais Magufuli kama mjasiriamali mwanamke kijana.
“Atupe nafasi tukutane naye wanawake wajasiriamali vijana kisha tutamweleza mengi yakiwemo ya kodi na mifumo yake, mimi ningemweleza haja ya vyombo vyote vya huduma kutumia mtandao, kutoa huduma ,ningemweleza haja ya halmashauri na taasisi kutoa mafunzo mbalimbali ili kuinua wajasiriamali hawa na kuwasapoti si tu kuchukua kodi na ushuru” anasema Mercy.
Anasema wajasiriamali wengi wadogo hawaendelei kwa kukosa sapoti ya mafunzo na namna ya kufanya biashara zao zikue.
“Wasiwe wanachukua kodi na ushuru tu, halmashauri hizi lazima zianze kufikiria kukuza wajasiriamali kwa kuwapa elimu inayostahili katika biashara zao” anasisisitiza Mercy ambaye amesema angelipenda kumuona Role Model wake (Rais Magufuli) kumweleza mengi yanayohusu wanawake vijana na viwanda vidogo kuelekea viwanda vikubwa na hamu ya wajasiriamali wanawake vijana kuchangia pato la taifa na kulipa heshima.
Anasema anapokutana na wajasiriamali wa Uganda, Rwanda anaona jinsi serikali zao zinavyowasaidia kunyanyuka na anaona serikali ya awamu ya tano inaweza kuwasikia na wao wakanyanyuka.

UVCCM MKOA WA ARUSHA WALAANI VIKALI SHUTUMA DHIDI YA MWENYEKITI WA CCM TAIFA

index
Na Mahmoud Ahmad Arusha
UMOJA wa vijana mkoa wa Arusha umelaani vikali kitendo cha jenerali Twaha ulimwengu kumkashifu Rais Mstaafu na mwenyekiti wa CCM taifa, Dkt Jakaya Kikwete kwa madai kuwa ashitakiwe mahakamani kwa kutumia fedha za umma vibaya kwa kuanzisha mchakato wa katiba ambao ulikwama kufikia tamati yake
 
Akitoa tamko hilio mbele ya wana habari mkoa wa Arusha mwenyekiti wa umoja wa vijana mkoa wa Arusha  Lengai Ole sabaya  alisema kuwa matamshi ya upotosha ji yaliyotolewa na jenerali twaha ulimwengu ni ya kupotosha umma
 
Aliongeza kuwa kutokana na matamshi hayo UVCCM wanamtaka jenerali aache kupotosha ukweli kama ulivyo kwani mchakato bado haujakwama ila umezingwa na miingiliano ya vipindi vya uitishaji wa kura ya maoni pamoja na kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
 
Aidha idhini ya matumizi ya fedha za mchakato wa Katiba ziliweza kuiidhinishwa na bunge kwa nia ya dhamira njema ya taifa ya kuandika katika yake mpya na wala sio ubadilifu au matumizi mabaya kama anavyotaka jenerali huyo.
 
Sabaya alisema kuwa alichokionesha jenerali mbele ya kadamnasi na vyombo vya habari ni kejeli pamoja na dharau isiyo staili kwani alionekana kujawa na nyongo kutokana na kumbukumbu zile za kuwekwa kando na utawala wa mkapa kasha kuzikwa kwenye kaburi la sahau utawala wa kikwete.
 
Aidha kutokana na matasmhi hayo umoja huo umewaomba na kuwasihi watanzania kuwa makini na kutuipilia mbali sanjari na kuweka tahadhari kwa watu wenye matamshi ya hamaki pamoja na hasira ambao wana nia mbaya ya kubomoa taifa.
 
Kutokana na hilo pia umoja huo umesema kuwa endapo kama ataendelea basi wao hawataweza kumtambua tena kama mwanachama mwenzao na pia watashinikiza hata uanachama wake utiliwe shaka kabisa

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG