![]() |
| Mmoja wa wagonjwa wa Akili |
![]() |
| Wauguzi katika hospital ya Mirembe |
![]() |
| Sehemu ya mji wa Dodoma |
![]() |
| Dodoma ipo katikati ya Nchi |
IMEANDALIWA NA BANDA BLOG
MGONJWA wa akili anayetibiwa katika
hospitali ya Milembe iliyopo mjini Dodoma Stella Mbalwa
amemuua mgonjwa mwenzake Halima chedi kwa kumpiga na kuni kichwani.
Akiongea na waandishi wa habari
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma ASP Lazaro Mambosasa alisema tukio hilo
lilitokea june 19 majira ya saa 3.30 asubuhi.
Kamanda alisema tukio hilo lilitokea
wakati wagonjwa hao wakinywa uji hospitalini hapo ambapo Stella alichukua moja
ya kuni zilizokuwa jirani na eneo hilo na kumpiga nayo marehemu kichwani ambapo
marehemu alipoteza maisha hapo hapo.
Wakati huo huo Kamanda Mambosasa
alisema Mwili wa mzee mmoja wa makamo anayekisiwa kuwa na umri wa kati ya miaka
70 na 77 ambaye hakutambuliwa jina wala makazi yake uliokotwa jirani na kanisa
la roma kata ya hazina manispaa ya Dodoma majira ya saa 2 asubuhi
Tags
AFYA



