Kufuatia
kuwepo kwa tatizo la mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo katika baadhi ya wakulima pia kushindwa kunufaika na mazao wanayozalisha,
hili pia halijawa jambo geni katika wilaya ya Kongwa ambapo August 3 2016 mkuu wa wilaya Deogratius Ndejembi alipoamua kupiga marufuku wafanyabiashara kuingia vijijini kununua mazao.
‘Jambo
la kwanza kuanzi sasa ni marufuku kwa mfanya biashara yeyote kuingia
vijiji vya ndani kununua mazao na akikamatwa afungwe hadi mimi niseme
atoke ‘ –Deogratius Ndejembi
‘Lapili nasitisha biashara yote ya mahindi, na viongozi husika mkishindwa kusimamia tutagombana‘ –Deogratius Ndejembi
‘Lakini
pia jambo la tatu ni kwamba biashara yote ya mahindi ihamie katika eneo
jengo lililojengwa kwa ajili ya kuuzia na kununulia, natoa siku saba
kwa soko lililojengwa na halmashauri kwa ajili ya biashara lianze
kutumika‘ –Deogratius Ndejembi
Unaweza kuendelea kumsikiliza hapo chini….
Tags
HABARI KITAIFA