BANDA MEDIA BLOG

HUENDA HII NDIYO SABABU YA KUSUASUA KWA MTIBWA SUGAR



YAHYA NJENGE

Baada ya kuona michezo ya ufunguzi ya Ligi Kuu ya Tanzania bara, kisima cha hisia zangu kimeguswa sana na matokeo yaliyo jitokeza pale Manungu Tuliani, kikosi cha Mtibwa Sugar kikichapwa bao moja kwa bila na Ruvu Shooting, Kwahakika rekodi za Mtibwa kwa miaka ya karibuni imekuwa ikifanya vizuri katika michezo ya awali lakini msimu huu hali ni tofauti.SPORTS.

TATIZO NI NINI?
Changamoto kubwa kwa Mtibwa Sugar ni kutolitumia vyema dirisha la usajili lililopita, Mtibwa wamejitengenezea utamaduni wa kuuza sana wachezaji wanao watengeneza na kila msimu wamekuwa wakibaki kwenye ubora wao, Hali ni tofauti kidogo msimu huu mtibwa imewapoteza wachezaji muhimu kama beki Andrew Vicent aliyeenda Yanga, Shiza Kichuya na Muzamiru Yasini waliojiunga na timu ya Simba.

Kwa hakika kupoteza mchango wa nyota hawa ni pigo la moyo kwa mtibwa, Nje ya nyota hao kocha waliyedumu naye kwa zaidi ya miaka mitatu Mecky Mexime nae ametimkia Kagera Sugar, Kwahakika kuondoka kwa kocha aliyeifahamu vizuri Mtibwa kutaitesa timu hii.SPORTS...

HATIMA YAKE
Ni mapema sana kusema chochote kwa sababu ni mchezo mmoja tumeona wamecheza chini ya kocha Salumu Mayanga, lakini wasipoangalia huu unaweza kuwa msimu mgumu zaidi kwao. Na kama walivyoshuka daraja vigogo Costal Union haitoshangaza na wao likiwakuta hilo.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG