BANDA MEDIA BLOG

DC MJEMA AWAIJIA JUU WANAOKODISHA MADAWATI




MOSHI SHABANI MALLEMA

Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imejitahidi kwa hali na mali kupitia wadau mbalimbali wa masuala ya Maendeleo, kufanikisha kuwa suala la uhaba wa madawati linakuwa historia kwa shule zote hapa nchini, ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam zoezi hilo limefanikiwa kwa kiasi cha kuwa na madawati mengine ya ziada, ambapo wilaya ya Ilala ina madawati ya ziada zaidi ya 3000, lakini kumekuwa na matumizi ambayo si sahihi kwa madawati hayo.DC MJEMA MADAWATI (1)

Akizungumza na Tovuti hii Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema ameeleza kuwa madawati yanayosambazwa na Serikali, kwenye shule mbalimbali hapa nchini ni kwa ajili ya wanafunzi pekee, hivyo yasitumike kwa matumizi mengine kama kukodisha kwa ajili ya shughuli za kisiasa, kidini na kijamii.DC MJEMA MADWATI  (4)

Huku akisisitiza kuwa Serikali inatumia gharama kubwa kwa ajili ya suala la madawati, hivyo kuyatumia madawati hayo kinyume na utaratibu ni kurudisha nyuma jitihada za Serikali katika kuwapatia elimu bora yenye mazingira rafiki watoto wa Tanzania, kwani madawati mengi yameripotiwa kuharibika kutokana na matumizi ya namna hiyo.KASSIM MAJALIWA CHAMAZI (2)

Ambapo amesema kuwa anapiga marufuku matumizi yasiyo rasmi kwenye madawati, ambayo yametengenezwa kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi ambao walikuwa wanateseka kwa kukaa chini, na kuahidi kuwachukulia hatua wote watakao kwenda kinyume na agizo hilo.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG