BURHANI MOHAMED
Wakicheza pungufu kwa muda mwingi wa
mchezo kufuatia kadi nyekundu aliyoipata kiungo wao Ally Hamisi Ng’anzi,
dakika ya 44 vijana wa Serengeti Boys waliigagadua Timu ya Taifa ya
Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Afrika kusini maarufu kama Amajimboz
mabao 2-0 yakifungwa na Mohamed Rashid Abdallah kipindi cha kwanza na
Muhsin Malima Makame kipindi cha pili.
Kwa ushindi huo sasa Serengeti Boys
wanasonga mbele hatua inayofuata kwa ushindi wa jumla wa 3-1 baada ya
sare ya 1-1 waliyoipata Afrika Kusini katika mchezo wa awali uliofanyika
wiki iliyopita.
Kwa ushindi huo ni kama Mwalimu Bakari Shime ametuma salamu kwa timu ya Taifa ya Vijana ya Congo ambayo yenyewe imeichapa Namibia 3-0 nakutinga hatua ya mwisho ya mchujo, ambapo watavaana na Serengeti Boys.
Tags
MICHEZO KIMATAIFA