Ripoti kutoka gazeti la Diario De Noticias kwamba Los Blancos wamegundua kwamba Bayern Munich walitaka kumsajili Garay akiwa Benfica, na waliweka ofa ya €15m mezani, ofa iliyokataliwa na klabu ya Ureno.
Hata hivyo, baada ya muda mfupi, Garay akauzwa kwenda Zenit kwa ada ndogo ya 6 million euros.
Garay, 29, ambaye aliihama Madrid kama sehemu ya dili la Madrid kumsaini Fabio Coentrao, Garay alijiunga na Madrid akitokea Valencia kwa €20m.
Kesi hii ya Madrid vs Benfica itatolewa maamuzi baadae mwezi huu na mahakama ya michezo duniani – CAS.
Tags
MICHEZO KIMATAIFA