BANDA MEDIA BLOG

Makamu wa Rais azindua kampeni ya Mti wangu

12
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza katika eneo la JKT Mgulani ambapo shughuli za uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti katika jiji la Dar es Salaam
zilifanyika.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Mhe. January Makamba akihutubia kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti iliyofanyika JKT Mgulani, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akihutubia wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwenye uzinduzi wa kampeni ya kupanda miti jijini Dar es salaam inayokwenda kwa jina la MTI WANGU iliyozinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka udongo katika mti alioupanda eneo la JKT Mgulani Barabara ya kilwa wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti katika jiji la Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akijiunga
na mtandao kwenye eneo la Gymkhana ambalo huduma ya WI-FI inapatikanika bure
kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
                                           ……………………………………………………………………………………….
Benjamin Sawe-Maelezo-Dar es Salaam
mefahamika kuwa hewa ya ukaa ina asilimia kubwa katika gesijoto hivyo kusababisha kumong’onyoka kwa ozoni na kupelekea kuongezeka kwa kiasi cha nyuzi joto duniani na udororaji wa uchumi wa nchi
Hayo yamebainishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa kampani ya upandaji miti ijulikanayo kama Mti Wangu katika mkao wa Dar e Salaam.
Mhe. Suluhu  alisema kwa kutambua athari za ongezeko la gesi joto hususani hewa ya ukaa serikali kupitia mkoa wa Dar es Salaam imekuja na kampeni ya kupanda miti ili kukabiliana na changamoto zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.
Alisema  mkoa wa Dar es Salaam unazalisha tani 4500 kwa kila siku zitokanazo na gesi za viwandani, vyombo vya usafiri, taka ngumu za viwandani na majumbani ikiwa ni pamoja na uchomaji na utupaji taka hovyo hivyo kupelekea serikali kwa kushirikiana na wadau kuanzisha kampeni hiyo jijini Daar es Salaam.
Alizitaja sababu nyingine za kampeni hiyo kuanzia Dar esSalaam ni pamoja na makadirio ya ongezeko la wakazi kufikia 5,895,791 kwa mwaka 2017 hivyo  kusababisha kuongezeka kwa kiasi kikubwa cha uzalishaji wa hewa ya ukaa kutokana na kuongezeka kwa mahitaji mbalimbali ya shughuli za binadamu na viwanda kwa ujumla.
Alisema tafiti mbalimbali zimeonyesha hewa ya ukaa inaongezeka jijini Dar es Salaam kutokana na ongezeko la viwanda na idadi kubwa ya wakazi ambapo kwa mwaka 2015 utafiti umeonyesha mkoa huo una viwanda 1854 kati ya hivyo 480 ni vikubwa na 1374 ni vidogo.
“Nawaagiza viongozi wa Serikali, taasisi binafsi, Asasi za kiraia na kila mtanzania kwa ujumla kutunza mazingira na kupanda miti ni hatua moja mbele katika kutunza mazingira yetu”.Alisema Mh. Suluhu.
Akimkaribisha mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hiyo, mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh. Paul Makonda alisema serikali imeweka chuma na minyororo ili kulinda wananchi kuvuka eneo ambalo si sahihi na kuweza kuhatarisha maisha yao kwa kugongwa na magari.
Alisema wananchi wanapaswa kulinda vyuma hivyo kwa kuwa vinasaidia kufanya mazingira yawe mazuri na kukinga miti na nyasi zilizopandwa kando ya barabara hizo zisiharibiwe.
“Wale wanaopita usiku na wale wanaoharibu, mtu yeyote akikamatwa ameiba chuma kimoja faini yake ni kununua vyuma kumi na kuchukulia hatua kwa mujibu wa sheria”.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG