BANDA MEDIA BLOG

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA,M HUKU WENYEWE WAKILIA UPUNGUFU WA DAWA

Makamu wa Rais Akiongea jambo wakati akifungua mkutano huo

Waziri wa afya Ummy Mwalimu akimakribisha Makamu wa Rais Kufungua mkutano huo


Mwenyekiti wa Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya Dkt, Sudi Leonard akisoma risala mbele ya makamu wa Rais Samia Suluhu [PICHA NA JOHN BANDA]

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana akizungamza kabla ya ufunguzi wa Mkutano huo


Wajumbe wa mkutano huo wakiwa katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere mjini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mkutano huo






Waganga wakuu wa mkoa na wilaya wakiwa na makamu wa rais katika picha ya pamoja
Majadiriano Baada ya picha ya pamoja


Na John Banda,Dodoma

WAGANGA  Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini wamemlilia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan kwa kudai tatizo la ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika baadhi ya vituo vya afya  nchini limekuwa likisababisha malalamiko wa Wananchi.

 Akizungumza katika Mkutano wa mwaka wa wataalamu wa sekta ya afya kwa niaba ya Waganga hao,Mwenyekiti wa Waganga hao,Dk Sudi Leonard alisema tatizo la ukosefu wa dawa na vifaa tiba limekuwa likisababisha malalamiko na manunguniko kwa wananchi.
‘’Mheshimiwa Makamu wa Rais pamoja na mambo yote lakini tunachangamoto ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba hali hii imekuwa ikisababisha malalamiko kwa Wananchi’’
‘’Mchakato wa upatikanaji wa dawa pia umekuwa ukichukua mchakato mrefu kutoka MSD mpaka kufika sehemu husika pia kuna hili kundi la watu maalum na wao wanapokosa hulalamika’’alisema   
Pia alisema kwa sasa wanaupungufu wa asilimia 49 ya watumishi na madaktari katika sekta ya afya hali ambayo huwalazimu kufanya kazi katika mazingira magumu.
‘’Tunaiomba serikali itoe fursa ya ajira kwani kwa sasa kuna Zahanati 334 ambazo zinasimamiwa na wahudumu ambao sio wataalamu wa afya’’alisema
Kwa upande wake Samia alisema kutokana na  tatizo la ukosefu wa dawa nchini serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 70 kwa ajili kumaliza tatizo hilo.
Samia alisema dawa hizo zitaenda moja kwa moja   katika vituo vya afya vilivyopo hapa Nchini.
‘’Tumetenga Bilioni 70 kwa ajili ya kumaliza tatizo la dawa nchini pia tumetenga jumla ya shilingi bilioni 85 kwa ajili ya kupunguza deni MSD nia yetu ni kutaka huduma za afya ziwe zenye ubora’’alisema
Pia alisema Serikali inampango wa kujenga Kiwanda cha dawa katika Mkoa ya Simiyu ili kuweza kukabiliana na tatizo la dawa hapa nchini.
‘’Tuna maombi ya viwanda kama 8 au 9 vya dawa na sasa tunahangaika kufungua kiwanda kikubwa cha dawa katika Mkoa wa Simiyu lengo likiwa ni kukabiliana na taizo la dawa pamoja na ile azma yetu ya Tanzania ya Viwanda
Vilevile aliitaka Wizara ya Afya maendeleo ya jamii,jinsia Wazee na Watoto kuhakikisha utafiti wa taaluma na dawa za asili zinazotumika nchini zinasajiliwa baada ya mamlaka husika kudhibitisha zinakidhi viwango.
‘’Tiba mbadala na tiba asili ni taaluma yenye asili ya kiafrika tuliyorithi kutoka kwa mababu zetu kutoka na uhitaji wake mkubwa   ninaagiza Wizara kuhakikisha waganga wa tiba asili wote wanasajiliwa na wanafahamika’’alisema
Pia aliwataka wataalamu hao wa afya kutosita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu wale wote wanaobainika kukiuka maadili na viapo vyao vya kazi.
‘’Niwatake wote kujitadhmini utendaji kazi wake na kubadilika mkubuke kuwa mustakabali wa afya za wananchi upo mikononi mwenu’’alisema
mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG