Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea hospitali ya mkoa wa Dodoma Oktoba 1, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akitoa maelekezo ya kuboresha usafi wa mazingira ya hospitali ya Mkoa wa
Dodoma wakati alipoitembelea hospitali hiyo Oktoba 1, 2016. Kulia
kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama. (Picha
na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akitoa maelekezo ya kuboresha usafi wa mazingira ya hospitali ya Mkoa wa
Dodoma wakati alipoitembelea hospitali hiyo Oktoba 1, 2016. Kulia
kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama. (Picha
na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na watumishi wa hospitali ya mkoa wa Dodoma baada ya
kutembelea hospitali hiyo Oktoba 1, 2016. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa
Dodoma Jordan Rugimbana. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya watumishi wa hospitali
ya mkoa wa Dodoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati
alipozungumza nao baada ya kuitembelea hospitali hiyo, Oktoba 1, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akimjulia hali Bi. Fatuma Yassin wa Swaswa Dodoma wakati alipotebelea
hospitali ya mkoa wa Dodoma Oktoba 1, 2016. Kushoto kwake ni Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akimjulia hali Bi. Magreth Kapinga wa Mpwapwa wakati alipotembelea
hospitali ya mkoa wa Dodoma Oktoba 1, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
……………………………………………………..
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amemuagiza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Ummy Mwalimu kuboresha upatikanaji wa huduma katika hospitali ya Rufaa
ya mkoa wa Dodoma kwa kuhakikisha inakuwa na dawa na vifaa tiba vya
kutosha.
Ametoa agizo hilo jana (Jumamosi,
Oktoba Mosi, 2016) wakati alipotembelea hospitali hiyo akiwa kwenye
ziara ya kukagua maeneo ya kutolea huduma za jamii mjini
Dodoma.
Waziri Mkuu amesema wakati
Serikali ikishirikiana na uongozi wa mkoa huo katika kumaliza changamoto
zinazoikabili hospitali hiyo manispaa nazo zinajukumu la kuboresha
utoaji wa huduma za afya katika zahanati na vituo vya afya.
“Waziri Afya atawajibika
kuimarisha hospitali ya mkoa na Manispaa waimarishe huduma katika
zahanati zote na vituo vya afya ndani ya mkoa kwa kuziwezesha kuwa na
majengo ya kutosha, kuongeza idadi ya watumishi na kuhakikisha zinakuwa
na dawa na vifaa tiba,” alisema.
Aidha, Waziri Mkuu aliwataka
watumishi wa hospitali hiyo kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu na
isitokee watu wakakosa dawa au vipimo kwa sababu mmoja wao amechukua na
kupeleka kwenye duka lake binafsi.
Pia Waziri Mkuu alimuagiza Mganga
Mkuu wa Mkoa Dk. James Kiologwe kutafuta vijana watakaoweza kusafisha
na kutengeneza bustani ya maua kwenye eneo lililoko karibu na uzio wa
hospitali hiyo ili liwe na mandhari ya kuvutia.
Awali Mganga Mkuu wa mkoa, Dk.
James Kiologwe aliiomba Serikali kupandisha hadhi hospitali hiyo na kuwa
ya kanda kwa sababu mbali ya mkoa wa Dodoma, hospitali hiyo inahudumia
wagonjwa wengine kutoka mikoa ya Iringa, Tabora, Singida na Manyara.
Akizungumzia upatikanaji wa tiba
wakati Serikali imeanza kuhamia Dodoma, Dk. Kiologwe alisema mkoa huo
unaweza kukabiliana na ongezeko la watumishi kwa una hospitali tano
ambazo zina madaktari bingwa wa fani mbalimbali.
“Tunazo hospitali tano ambazo ni
Benjamin Mkapa, Mirembe, DCMC, St. Gemma na hii ya ya Rufaa ya Mkoa
zenye uwezo wa kutoa huduma za upasuaji, huduma kwa mama na mtoto,
magonjwa ya moyo, mishipa, figo na saratani na huduma za mionzi,”
alisema.
Katika hatua nyingine Dk.
Kiologwe alisema hospitali hiyo imedumia wagonjwa wa nje 158,375
walipatiwa huduma katika hospitali hiyo katika kipindi cha Julai 2015
hadi Juni 2016 ambapo ni sawa na wastani wa wagonjwa 13,198 kwa mwezi.
“Magonjwa yanayoongoza kwa
wagonjwa wa nje ni mivunjiko, shinikizo la damu, kisukari, homa ya
mapafu na upungufu wa damu,” alisema.
Tags
AFYA